14 wafariki huku visa vipya 606 vya coronavirus vikisajiliwa

kagwe 1
kagwe 1
Kenya leo imesajili visa vipya 606 vya coronavirus na kufikisha jumla ya visa hiyo nchini kuwa   18,585

Visa hivyo ni kutoka sampuli 4,888  zilizopimw akatika saa 24 zilizopita .

Waziri wa afya Mutahi Kagwe  amesema watu 409 ni wanaume ilhali 197 ni wanawake .mgonjwa aliye na umri wa chini sana ana miezi minne  ilhai mwenye umri wa juu ana miaka 85.

Watu 75 wamepona kutokana na ugonjwa huo na kufikisha  7,908 watu waliopona corona hadi kufikia sasa .

Kagwe amesema wanaofanyia kazi nyumbani wanafaa kuhakikisha kwamba wanafanyia katika nyumba zao .

"  Nimekuwa risasi nawe pia umekuwa risasi ,tumekuwa hatari na  tunaweza kusababisha maafa’ amesema Kagwe

Amewahimiza wazazi kuhakikisha kwamba wanapo wananawa mikono kila wakati

Kagwe  amekariri msimamo  wa rais Kenyatta kwamba hakuna atakayesazwa  katika kuhakikisha kwamba kila mmoja anafuata kanuni zilizowekwa kuzuia usambaaji wa virusi vya corona .

Amewashauri watu kutosafiri kwenda  mashambani  ama kuwaalika wageni makwao isipokuwa katika hali za dharura .