Unyama:Mwanamke awaua wanawe wawili Nandi

Mwanamke mmoja amewaua watoto wake wawili kwa kuwakata kata  katika tukio la kutisha huko nandi na kisha kutoroka . mshukiwa aliuwa wasichana  hao walio na umri wa miaka 11 na saba  kabla ya kuwakatakata vipande na kuitupa miili yao katika  shimo la futi 30  la choo .

 Mkusanyiko wa Habari na Matukio Muhimu ...

Oparesheni za kampuni za michezo ya kubashiri sportpesa zinaendelea ikiwemo matumizi ya nambari zake za malipo  kufuatia agizo la mahakama linawaruhusu kuendelea na  shughuli zao .wakili Joan Kiarie  amesema agizo la serikali kuondoa nambari hizo na kuongeza ushuru ni hatua inayoavuruga biashara za michezo ya kubashiri ilhali wametekeleza sheria zote .

Mwanamke mmoja raia wa Rwanda  amehukumiwa  kifungo cha miaka miwili jela kwa kumwua mumewe ambaye ni mkenya . anashtumiwa kwa kumwua mumewe wakati walipokuwa wakingomabana  baada ya marehemu kusemakwamba alitaka kuoa mke wa pili  korti ilipunguza shtaka lake kuwa la mauaji ya kutokusudia .

Wazazi ndio wanaofaa kulaumiwa kwa ongezeko la visa vya wasichana  wadogo kutungwa mimba huko kilifi na sio wahudumu wa boda boda . waziri wa jinsia wa kaunti    Maureen Mwangovya  amesema wahudumu wa boda boda wamekuwa wakitwika lawama ambayo sio yao .

Mbinu ya sasa ya mtu kutangaza wazi mali yake sio ya kuaminika  na haiwezi kutegemewa katika vita dhidi ya ufisadi .afisa mkuu mtendaji wa tume ya EACC Twalib Mbarak  amesema wanapendekeza marekebisho ya sheria ili kufanya zoezi hilo kuwa la kielektroniki  ndiposa waweze kupata maelezo ya mapato,mali na madeni  ya maafisa wa serikali .

Tume ya kupambana na ufisadi EACC imerejesha mali yenye thamani ya shilingi bilioni 2.7 katika kipindi cha miezi minne iliyopita .afisa makuu mtendaji Twalib Mbarak  amesema fedha hizo zilirejeshwa kupitia njia mbadala ya kusuluhisha mizozo  .

Aliyekuwa mkuu wa utumishi wa umma Francis Muthaura  ameunga mkono pendekezo la kuwateua wabunge kama mawaziri . muthaura amesema kuwazuia wabunge kuhudumu kama mawaziri ni jambo ambalo limezua uhasama kati ya  viongozi wa kisiasa na  viongozi wengine utawala wa serikali .

Kampuni za maji taka zimehimizwa  kuhakikisha kwamba  maeeo ya kutupa taka hayawi karibu na vyanzo vya maji ili kuepuka kuyachafua maji . mtaalam wa afya ya umma Josephine Ofdanga  amekushauri kuhakikisha kwamba unaweka dawa au kuyachemsha maji unayotumia .

Kufaulu au kufeli kwa ndoa yako hakutegemi iwapo una cheti cha ndoa .mtaalam wa masuala ya uhusiano wanjiku waititu  amesema jinsi unavyojitayarisha kwa ndoa ndio msingi wa iwapo itafulu au la .

Eneo la kuosha na kurembesha magari la Pimp my ride limebomolewa  baada ya mahakama kuipa city hall ruhusa ya kufanya hivyo . aeneo hilo la kusafisha magari ambalo limejengwa upya mwezi uliopita  ,lilibomolewa mwendo wa saa tano usiku . maafisa wa city hall mwezi mei walikuwa tena wamelibomoa eneo hilo wakisema limejengwa bila idhini .