Joseph Kori amekosa kutoa ushahidi dhidi ya mpenzi wake wa pembeni Judy Wangui kuhusu mauaji ya mkewe kwa sababu ya hitilafu ya ushahidi . Kori atafika kizimbani juni mwaka ujao kutoa ushahidi dhidi ya Wangui .awali alikuwa amekamatwa kuhusiana na mauaji hayo lakini sasa ni shahidi wa serikali .
Eneo la kivuko cha feri limetangazwa kuwa eneo maalum la oparesheni ya kijeshi na wananchi hawaruhusisi kufika hapo huku shughuli ya kuitafuta miili ya Mariam kighendi na mtoto wake ikiendelea . mwenyekiti wa bodi ya huduma za feri Dan mwazo amesema eneo hilo sasa lipo chini ya jeshi la majini na shirika la feri .
mbunge wa Mvita Abdulswamad Nassir amesema maandamano dhidi ya reli ya SGR yataenfdelea licha ya wanadamanaji kutupiwa vitoa machozi hivi leo . amesema serikali iliwadanganya kwamba imefutilia mbali agizo kwamba mizigo yote kutoka bandari isafirishwe kutumia SGR ilhali huko mashinani wangali wanalazimishwa kutumia usafiri wa reli .
Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi amewashtumu mbunge mteule maina kamanda katibu wa utawala Rachel Shebesh na spika wa bunge la Nairobi Beatrice Elachi kwa kukiyumbisha chama cha jubilee .Sudi amesema rais uhuru Kenyatta anafaa kuwachukulia hatua watatu hao ambao wamekuwa wakitoa matamshi ya uchochezi .