Habari Muhimu ,Toleo la saa Saba 15/10/2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC
Madreva wa magari ya kibinafsi bado ndio  hatari katika baraara zetu .takwimu  kutoka NTSA  zinaonyesha kwamba  magari ya kibinafsi yalisababisha vifo vya watu 722 kati ya januari na oktoba mwaka huu  ikilinganishwa na watu 630 waliouawa na magari ya kibiashara . madreva wa matatu walisababisha vifo vya watu 415 ikilinganishwa na watu 433  mwaka jana .

Uteuzi wa mbunge wa zamani wa Othaya Mary wambui kama mwenyekiti  maamlaka ya ajira umezua lalama  kali sana mtandaoni kutoka kwa wakenya na hasa katika ukumbi wa twitter .wengi wamehoji nia ya serikali kumpa wambui kazi hiyo kwani   suala la ajira linazua hisia kutoka kwa vijana wengi nchini ambao wamezua shauku iwapo wambui  ana uwezo wa kutoa na kutekeleza sera na mikakati bunifu ya kuwawezesha vijana kupata kazi .waziri wa leba Ukur Yattani alitangaza uteuzi wa wambui katika maamlaka hiyi kupitia arifa maalum ya gazeti rasmi la serikali hapo jana .

Mwanamikakati wa mawasiliano wa kidijitali Dennis Itumbi na shahidi Samuel gateri wameshtakiwa upya kuhusiana na barua feki iliyodai kuwepo njama ya kumwua naibu wa rais William Ruto . wawili hao wamefikishwa kortini leo baada ya upande wa mashtaka kuziunganisha kesi zao . wamekanusha  mashtaka ya kuchapisha  taarifa ya wongo kinyume cha sheria .

Mkurugenzi wa mashtaka ya umma  amewasilisha kesi ya ukiukaji wa agizo la mahakama dhidi ya mjane wa TOB COHEN SARAH WAIRIMU NA wakili wake Philip Murgor . DPP anasema wawili hao wanafaa kuchukuliwa hatua kwa kuzungumzia mauaji ya COHEN wakati wa maazishi yake .

Afisi ya mratibu wa bajeti imekashifiwa leo na maseneta  kuhusu kutolewa kwa pesa kwa njia isiofaa kwa ununuzi wa vifaa vya  matibabu katika hospitali za umma . aliyejipata pabaya ni kaimu mratibu wa bajeti Stephen Masha .

  Bunge la kaunti ya meru leo linajadili mswada wa punguza mizigo .mswada huo hadi kufikia sasa umekataliwa na kaunti 16  na ni uasin Gishu pekee ndio iliyoupitisha .

Rais wa zamani wa afrika kusini Jacob Zuma  atakata  rufaa  katika kesi ya ufisadi dhidi yake   baada ya mahakama wiki jana kutupilia mbali ombi lake kwamba kesi hiyo ifutiliwe mbali . Madai ya ufisadi dhidi ya Zuma ni  ya miaka ya 90 wakati taifa hilo lilipotoa kandarasi ya ununuzi wa sulaha .Hilo linajiri  baada ya marekani wiki jana kuiwekea vikwazo familia ya Gupta  na mshirika wao mmoja kwa tuhuma za ufisadi nchini afrika kusini . Familia ya Gupta ilikuwa na uhusiano wa karibu na Zuma na utawala wake.