Watahiniwa wote waliosajiliwa kufanya mtihani wa KCPE wataufanya mtihani huo .waziri wa elimu George magoha amesema hakuna mtahiniwa atakayezuiwa kuufanya mtihani huo kwa sababu ya kudaiwa karo .
Waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi amewaonya walimu dhidi ya kucheza kamari na maisha ya wanafunzi .hii ni baada ya kuliona dari la darasa moja lilikikaribia kuanguka katika shule ya msingi ya GILGIL nys ambako alikuwa anasimamia oezi la kuanza kwa mtihani wa KCPE .
MvUA itaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali ya taifa katika siku tano zijazo . Stella Aura kutoka idara ya utabiri wa hali ya anga amesema kiwango cha mvua kitazidi kuanzia siku ya jumanne . maeneo yakatoyopokea kiasi cha cha zaidi ya milimita 30 ya mvua ni pamoja na Siaya, Kisumu, Homa Bay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia ana Baringo .
Mahakama imefutilia mbali kutekelezwa kwa arifa iliyotolewa na wizara ya fedha kupunguza bajeti ya idara ya mahakama . CHAMA CHA LSK ndicho kilichowasilishwa kesi hiyo kortini na kimeagizwa kuzikabidhi pande husika uamuzi huo huku kesi yenyewe ikitarajiwa kutajwa Novemba tarehe 6 kwa maelekezo zaidi .
Mtihani wa KCPE Umeanza VYEMA KATIKA MAENEO MENGI YA TAIFA .KONTENA ZA mtihani huo hapa jijini na mombasa ziluifunguliwa kwa wakati .huko Mombasa ,waziri wa elimu George Magoha alikuwa katika shule ya msingi ya mwangala mtaani likoni kushuhudia zoezi la kufunguliwa kwa mtihani
Hata hivyo mtihani huo ulichelweshwa katika baadhi za sehemu zikiwemo kwale ,baringo turkana magharibi na west pokot kwa ajili ya mvua kubwa .
Huku hayo yakiarifiwa ,watahiniwa wanne wa KCPE katika shule za msingi za Kyunguni na kasikeu huko Mukaa hawatafanya mtihani wa mwaka huu wa KCPE BAADA YA MAjina yao kukosekana katika sjaili ya watahiniwa .huyu hapa kamishna wa kaunti Maalim Mohamed .
Mfanyibiashara Peter Karanja ameachiliwa kwa bondi ya shilingi milioni nne au dhamana mbadala ya shilingi milioni 2 pesa taslimu . Karanja ameshtakiwa kwa mauaji ya bwenyenye Tob Cohen .jaji Daniel Ogembo amemwagiza karanja kutokaribia boma la Cohen na pia kusalimisha paspoti yake kortini .
Kampuni ya Kenya Power imemteua Bernard Ngugi kama maneja mkurugenzi ili kuichukua nafasi hiyo mara moja .kabla ya uteuzi wake ,Ngugi amekuwa akihudumu kama maneja mkuu wa uagizaji .Anaichukua nafasi hiyo kutoka kwa Jared Othieno ambaye amekuwa akihudumu kama kaimu maneja mkurugenzi .
Maafisa wawili wakuu katika idara ya usajili wa watu wamesimamishwa kazi kuhusiana na tuhuma za ufisadi .waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi amesema wawili hao wametajwa katika visa vingi vya ulaji rushwa ambavyo vimelipaka doa idara hiyo .
Mwakilishi wa wanawake kaunti ya Taita Taveta Lydia Haika amewataka wakazi wa kaunti hiyo kumkea na kutomsikiza gavana Granton Samboja na wawakilishi wadi kwenye mikutano watakayoandaa hadi pale watakapo suluhisha mzozo wa bajeti unaoendelea.Haika anasema kuwa tofauti kati ya pande hizo mbili zimelemaza maendeleo hali anayosema kuwa imeumiza pakubwa wakaazi