Visa hivyo ni kutoka sampuli 3,307 zilizopimwa katika saa 24 zilizopita . visa vyote ni vya wakenya isipokuwa 7 .
Idadi ya walioaga dunia kwa ajili ya Covid 19 sasa imefikia watu 669 baada ya watu watano kuaga dunia .
Mwangangi amesema mgonjwa wa umri wa chini ni mtoto wa miaka mine ilhali wa umri wa juu ana miaka 74 .
Kaunti ya Trans Nzoia kwa mara ya kwanza inaongoza kwa visa vingi baada ya kusajili visa 28 katika saa 24 zilizopita .
Nakuru ina visa 24, Nairobi 14, Migori 8, Turkana 5, Bungoma 2, Murang'a, Busia, Nyeri na Vihiga zina kisa 1 kila moja
Watu wengine 81 wamepona na kufikisha idadi ya waliopona ugonjwa huo kuwa 24,334.
Kiwango cha uponaji wa ugonjwa huo nchini sasa kimfikia asilimia 65 . Mwangangi amesema ingawaje kenya imefaulu kupunguza maambukizi ya virusi hivyo,ugonjwa huo bado hauna tiba