Msichana aliyepona virusi vya Corona na kutumiwa na serikali kama kielelezo cha kuondoa hofu kuhusu virusi hivyo Brenda Cherotich amejipata pabaya baada ya wanamitandao kuanza kumsaga kote huku picha zake akiwa uchi pia zikianikwa peupe .
Kando na familia yake kuwa na wakati mgumu baad ya binti yao kuambukizwa virusi hivyo ,wamejipata tena katika mashaka mengine kujaribu kuwazuia wanamitandao kumuingiza kichaa mrembo huyo ambaye wengi walianza kutilia doa masimulizi yake kuhusu jinsi alivyopata ugonjwa huo .
Babake Brenda Peter Rono amesema familia yake kwa sasa ipo katika tahadhari ili kumuzia binti yake asiambukizwe tena virusi hivyo . Amesema familia hiyo haitaanda karamu ya makaribisho huko Ainamoi kwa sasa ili kuzuia mkusanyiko wa watu wengi .
Bwana Rono pia anahofia usalama wa mwanawe mwingine wa kiume ambaye yupo nchini Marekani lakini hajapatikana na virusi hivyo.