Soma mengine hapa:
Katika kikundi hicho, alitokea jamaa na kibuyu cha lita 5 za pombe na noti ya shilingi moja mkononi.
‘Atakayemaliza pombe hii nitamkabidhi shilingi elfu moja,” aliwaeleza marafiki zake.
Mwendeshaji bodaboda alitokea na kwa ujasiri akachukua kibuyu hicho cha chang’aa na kumaliza pombe yote. Dakika chache ata kabla apewe zawadi yake kuu ya elfu moja ,alianguka na akazirai. Marafiki wenzake walimbeba hobelahobela na kumpeleka nyumbani kwake. Alionekana mnyonge na kupumua kwa nguvu sana.
Soma hapa:
Marafiki wake walimwacha apumzike na siku ilyofuata wakafika kumwona na kumjulia hali mwenzao. Cha kustaajabisha ni kuwa walimpata ameiaga dunia kwani hakuna mtu angemsaidia katika chumba kile. Kwa mujibu wa taarifa za vyanzo vinavyoaminika,pombe aliyoikunywa ilimzidia na kumfanya afariki.