Mcheshi Erick Omondi amekuwa kimya zaidi katika mitandao ya kijamii siku za hivi karibuni, na alipokuwa kwenye mazungumzo na mojawapo ya stesheni za humu nchini, alisema kuwa amekuwa akifanya baadhi ya kazi mpya ambazo zitawafaa wafuasi wake.
Omondi aidha alitokeza kuwa mkurupuko wa virusi vya Corona umefanya watu wengi kusalia kwa nyumba zao kwa hofu ya kuambukizwa virusi hivyo.
Kutokana na kukua kwa teknolojia haswa mitandao ya kijamii, mcheshi huyu aliamua kufanya video iliyowaacha wengi wakiwa vinywa wazi, wengi wakiwa wanawake waliofurahishwa na jinsi Omondi alivyokuwa ananengua kiuno chake hali iliyowafanya baadhi yao kumtania kuwa anawapa hamu ya kushiriki twa twa.
Wengine walimpongeza kwa kuongeza uzani baada ya miaka mingi ya wafuasi wake kumtania jinsi alivyokuwa mkonde.
Liz: Omosh umenona ama ni nguo umevaa mob😂😂😂
Edwards: Ni kweli amemuona sana! 😂
Racheal: Naona umenona kila mahali pa maana 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Famran: Umenona mzae Quarintine inakupeleka poa
Wanjiru: Umeanza kunona uso aki😂😂😂😂
Mary: He’s become so cute
Ann: Na umenona akii😱😱😱 @ericomondi
Riodee: @ericomondi naona umeanza kukula vizuri…uso💪🏿💪🏿💪🏿💪🏿