Aki Erick unatupa hamu ya twa twa! Wanawake wachizi baada ya kuona mnenguo wa Erick Omondi

NA NICKSON TOSI

Mcheshi Erick Omondi amekuwa kimya zaidi katika mitandao ya kijamii siku za hivi karibuni, na alipokuwa kwenye mazungumzo na mojawapo ya stesheni za  humu nchini, alisema kuwa amekuwa akifanya baadhi ya kazi mpya ambazo zitawafaa wafuasi wake.

Omondi aidha alitokeza kuwa mkurupuko wa virusi vya Corona umefanya watu wengi kusalia kwa nyumba zao kwa hofu ya kuambukizwa virusi hivyo.

Kutokana na kukua kwa teknolojia haswa mitandao ya kijamii, mcheshi huyu aliamua kufanya video iliyowaacha wengi wakiwa vinywa wazi, wengi wakiwa wanawake waliofurahishwa na jinsi Omondi alivyokuwa ananengua kiuno chake hali iliyowafanya baadhi yao kumtania kuwa anawapa hamu ya kushiriki twa twa.

Wengine walimpongeza kwa kuongeza uzani baada ya miaka mingi ya wafuasi wake kumtania jinsi alivyokuwa mkonde.

 
 Hapa ni baahi ya maoni ya mashabiki

Liz: Omosh umenona ama ni nguo umevaa mob😂😂😂

Edwards: Ni kweli amemuona sana! 😂

Racheal: Naona umenona kila mahali pa maana 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Famran: Umenona mzae Quarintine inakupeleka poa

Wanjiru: Umeanza kunona uso aki😂😂😂😂

Mary: He’s become so cute

Ann: Na umenona akii😱😱😱 @ericomondi

Riodee: @ericomondi naona umeanza kukula vizuri…uso💪🏿💪🏿💪🏿💪🏿