Akothee asema kuwa yuko tayari kupata mtoto wa sita

akothee pant outfit
akothee pant outfit
Mwanamziki mwenye utatanishi mwingi hapa nchini, Akothee, amesema kuwa atakuwa mama wa watoto sita kabla afikishe umri wa miaka 40.
"Sisi tunataka kutembea ulimwenguni kote kabla tufikishe umri wa miaka 40 kwa sababu wakati huo ntakuwa na mtoto wa sita. Cjui  Zari naye yuataka nini ila nafikiria pia yeye yupo ndani. Kwa sasa kazi ni kutembea na kujipa likizo,"

Akothee aliandika kwenye mtandao wake wa instagram.

 Akothee kwa sasa ni mama wa watoto watano na anasema kuwa anataka kumaliza mambo ya uzazi kabla afikishe umri wa miaka 40. Kwa sasa, Akothee ana umri wa miaka 38 na ndani ya miaka miwili atakua na umri wa miaka 40.

Ikumbukwe kwamba Akothee amekuwa akieneza uvumi kuwa sio lazima mwanamke aolewe ili kuwa na maisha mema. Hata hivyo, mambo huenda yamebadilika raudi hii kwani aliongeza kuwa,

" Mie kwa sasa nataka kuoleka na nitulie na bwana yangu. Ningependa sana kupata mwanaume."

Akothee hivi majuzi pia aliweka ujumbe mtandaoni akieleza kwamba yuataka kuolewa kisha atulie na maisha yake.