Video hiyo ya wimbo ‘Dodo’’ inaeleza hafla ya harusi huku Hamisa akiwa ndiye mhusika mkuu katika masimulizi ya wimbo huo .
Itakumbukwa kwamba Ali kiba na Diamond wana bofu ambayo imekuwa wakati mwingine inazima na kulipuka na
ni kinaya kwamba Hamisa naye ni 'baby mama' wa Diamond kwani walikuwa wapenzi awali na wana mtoto. Katika wimbo huo, Ali Kiba anaeleza jinsi anavyompenda Hamisa(Hatujui Simba atasemaje kuhusu hilo)
’
“Kupenda ni vitendo si maneno maneno, leo nakupa kitengo kwa kufika Malengo, umeziba Mapengo, kwa upendo upendo, Bora wanazengo anze vikao vya sendoff Eeeh, Maa’ inashuka mistari hiyo
Anaongeza Kiba ;
‘Maana we mrembo nakujuzaaah..mama nashukuru umekuza, chanda kama pete nitakutunza … na umeshanizimaa, ayoyoyooo Love, ayoyoyooo my love, ayoyoyooo Love, your love, Dodo langu Beibe,” Ali Kiba anafoka mistari hiyo katika wimbo wenyewe
Mashabiki wengi walionekana kumsifia Kiba kwa kuamua kumtumia Hamisa katika video ya wimbo huo
presenterdmike “Hakika @hamisamobetto ameitendea haki Video ”
ridhonekigu_ ‘King of tanzania big up bro ”
lumiere_mbilizi ‘Ye baba! Afu nimemuona @hamisamobetto ndo imenoga zaidi…”
officialgerard_hero ‘Huu Unyama wa mama DAYLAN NOMA Sijui Itakuaje kule ”
ally__kiba “Hii Video haijawahi tokea hapa Tanzania tangu dunia iumbwe sasa mtu ukibisha ruksa kunya boga ama tikiti #DODO Video link on bio!!… ”
c.g.englibert ‘Shkamoo baba…. kupenda Ni vitendo si maneno maneno :