Aliyekuwa mshambulizi wa Ghana aiaga Dunia

Aliyekuwa mshambulizi wa Nottingham forest na timu ya taifa ya Ghana, Junior Agogo ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 40 kutokana na ugonjwa wa  Kiharusi.

Agogo alichezea taifa la ghana mara 27 kwenye mechi za kimataifa huku akicheka na wavu mara 11 maishani mwake. Alianzia soka yake na klabu cha Shefield United kabla ya kwenda nchini Marekani. Baadaye alirejea nchini Uingereza na kuchezea Brentford pamoja na Nottigham Forest.

Agogo alitetemesha ulimwengu wa soka akichezea klabu cha Bristol City. Vilabu alivyochezea vimesikitikia kifo chake na kutumia familia yake risala za rambi rambi.

Amekuwa akiugua maradhi ya kiharusi tangia mwaka wa 2015.