Aluta Continua:Miguna Awashtaki maafisa 25 wakuu wa serikali kuhusu uraia wake .

Wakili Miguna miguna amewashtaki maafisa 25 wakuu wa serikali  kwa anachokitaja  kama  kumnyima uraia wake wa Kenya . Walishtakiwa na Miguna ni pamoja na   waziri Fred Matiang'i,  Mkuu wa sheria , mkurugenzi wa idara ya uhamiaji ,mkuu wa DCI , mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma , na katibu katika  idara ya uhamiaji .Miguna  siku ya ijumaa alisema kwamba ni raia  wa Kenya mzaliwa wa taifa hili na alifurushwa nchini kinyume na matakwa yake  na hajawahi kusalimisha uraia wake wa Kenya .

Aliongeza kwamba alikuwa kiongozi wa wanafunzi katika chuo kikuu cha Nairobi mwaka wa 1987  na aliteswa mwaka huo na vyombo vya usalama nchini kwa  kujihusisha na shughuli a kisiasa .Miguna  Miguna amesema hakusafiri kwa hiari kwenda Canada kutoka Kenya  na hajawahi kuukana uraia wa Kenya . Serikali ilimtimua Muguna nchini mwaka jana  kwa madai kwamba alipewa paspoti ya Kenya kinyume cha sheria .

“ Wakati Miguna alipopewa paspoti ya Kenya  kinyume cha sheria alikuwa  akifanya kazi katika afisi ya waziri mkuu kama mshauri wa Raila Odinga’ ilisema taarifa ya serikali .Miguna  ameipuuza taarifa hiyo ya serikali akisema kwamba alilazimika kukimia mafichoni  kwa sababu ya hofu ya uwezekano wa kushtakiwa  na hakuondoka Kenya kwa hiari. Amesema maafisa hao 25 wa serikali waliiharibu paspoti yake  na vifaa vyake  kabla ya kumfurusha kwa lazima nchini bila notisi yoyote .