logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rafiki wa Jowie avunja kimya baada ya kuhukumiwa kwa rafiki yake

Rafiki wa Jowie Hamez Githinji kama anavyojiita Instagram,  alishtua mashabiki  kwa alichochapisha katika instastories zake kuhusu mauaji ya Monica Kimani.

image
na Davis Ojiambo

Burudani14 March 2024 - 11:45

Muhtasari


  • kwa alichokipost, ilionekana rafiki yake Jowie alificha ukweli na alikuwa akimlinda mtu ambaye labda alihusika na uhalifu.

Rafiki wa Joseph Irungu "Jowie", Hamez Githinji kama anavyojiita Instagram,  alishtua mashabiki  kwa alichochapisha katika instastories zake .

kwa alichokipost, ilionekana rafiki yake Jowie alificha ukweli na alikuwa akimlinda mtu ambaye labda alihusika na uhalifu.

"Iligharimu kiasi gani kubeba msalaba wa mtu kaburini kwako?? Walikuahidi watakutoa?? kiri ukweli jamani!!

Pia alimhakikishia jowie kwamba anaweza kuomba tena hukumu hiyo.

"Unaweza kuomba tena hukumu hiyo... Tafadhali iambie dunia ukweli... Unajua ni nani aliyefanya hivyo??...

Chapisho lake lilipata maoni tofauti tofauti  kutoka kwa Wakenya. Wengine waliamini kuwa Jowie hakutenda kosa, wengine wakidhani kuwa anaongea tu huku wengine wakiuliza kwanini ameamua kuongea sasa hivi kujaribu kumwokoa rafiki yake.

Mwezi uliopita Jowie alipatikana na hatia ya mauaji ya Monica Kimani, ambaye aliuawa kikatili katika nyumba yake ya Lamuria Gardens jijini Nairobi usiku wa Septemba 19, 2018.

Hakimu Nzioka aliamua kuwa upande wa mashtaka ulitoa ushahidi wa kutosha na kuthibitisha bila shaka kuwa Jowie kweli alimuua Monica.

Akitoa uamuzi huo Jumatano, Jaji wa Mahakama Kuu Grace Nzioka alisema mauaji ya kutisha ya Monica Kimani yalikuwa ya "kusudi."

"Mauaji yanaacha nyuma njia ya ndoto zilizovunjika na mioyo iliyovunjika ambayo haiwezi kuponywa."

"Kitendo cha mauaji ni uhalifu wa kutisha ambao unapinga muundo wa maadili wa jamii na unadai haki," Grace Nzioka alieleza mahakama.

Jowie hivi sasa amehukumiwa kifo baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani 2018.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved