In Summary

• Mamlaka ya Afya ya Jamii, Social Health Authority, yaani SHA, iko hapa kuleta mabadiliko.

• Mtu yeyote anayeishi nchini Kenya anafaa kujisajili upya na Social Health Authority hata kama alikuwa amesajiliwa na NHIF.

• Jisajili kwa kubonyeza *147# au kupitia www.sha.go.ke.

Watu  wengi wanatatizika kwa sababu ya kukosa huduma bora za afya. Baadhi yao ambao wanaugua wamekosa tumaini.

Mamlaka ya Afya ya Jamii, Social Health Authority, yaani SHA, iko hapa kuleta mabadiliko.

SHA ilibuniwa ili kurahisisha na kupunguzia Wananchi mzigo wa gharama za matibabu.

Mtu yeyote anayeishi nchini Kenya anafaa kujisajili upya na Social Health Authority hata kama alikuwa amesajiliwa na NHIF.

Jisajili kwa kubonyeza *147# au kupitia www.sha.go.ke.

Wananchi pia wanaweza kujisajili kwenye kituo cha afya cha serikali kilicho karibu nao,au tawi la SHA au katika vituo vya Huduma Centre.

Je ni huduma zipi utakazo pata kupitia SHA

Kupitia SHA utapata huduma za kutibiwa na kurudi nyumbani (outpatient), kulazwa, huduma za kujifungua, matibabu ya watoto, Matibabu ya maradhi ya figo, Afya ya akili, Huduma za Upasuaji, Saratani,  X ray na Huduma Zingine za Uchunguzi, Matibabu ya nje ya nchi na magonjwa mengine.

Kuanzia uchunguzi wa maradhi na kinga hadi matibabu maalum, SHA itahakikisha unalindwa wewe na familia yako dhidi ya gharama kubwa za matibabu.

Kila Mkenya anastahili kupata huduma bora za afya. Hakuna mtu anayepaswa kukabiliwa na changamoto za kifedha kwa sababu ya magonjwa.

Jiunge na SHA ili huduma ya afya iwe ya maana kwako, familia yako, na jamii yako. Jisajili na Mamlaka ya Afya ya Jamii ya SHA leo.

 

Mamlaka ya Afya ya Jamii ya SHA – Bima Bora, Afya Nyumbani.

View Comments