Lebo ya wasafi ina kipusa mpya, Zuchu ambaye amekuja kwa kasi na nguvu zote. Zuchu amejiunga na lebo hiyo ya msanii Diamond Platinumz na ni binti yake mwanamuziki maarufu wa taarab kutoka Bongo Khadija Kopa.
Kupitia kumbi zao za mitandao ya kijamii WCB wamemtambulisha Zuchu kwa mashabiki wao kwa kuandika ;
WE INTRODUCE TO YOU THE NEW QUEEN OF BONGO FLEVA||
ZUCHU Ni mtoto wa Malkia Mwenye Sauti ya Kasuku @khadijakopa.
Amepikwa akapikika
Sasa Ni Muda wa Dunia Kufurahia kipaji Hiki Kipya kutoka Tanzania.
Ladies & The Gentleman Rasmi Tunamtambulisha Kwenu Msanii Mpya @officialZuchu Katika Label Yetu Ya @wcb_wasafi .
Tafadhali kwa Heshima na Taazima Tunawaomba Watanzania Mumpokee na Kusheherekea Kipaji chake. .
#TheNewQueenOfBongoFleva #KaribuZuchu #WelcomeZuchu
#Wcb_wasafi
#WCB4LIFE
Cc @boomplaymusic_tz
Mtazame Malkia huyu anayeleta sauti freshi katika bongo fleva
MHARIRI: DAVIS OJIAMBO