Arsenal vs Man City: Baada ya kupokea kichapo dhidi ya Man United, Guardiola ataandikisha ushindi leo?

Klabu ya Manchester City hii leo watakuwa wanachuana na klabu ya Arsenal Ugani Fly Emirates. Ni mechi ambayo mashabiki wa soka wamengoja kwa hamu  lengo likiwa kuthibitisha nani bora zaidi.

Man City waliweza kupoteza mechi dhidi ya Man United wikendi iliyopita nyumbani kwao Etihad baada ya bao ya Marcus Rashford na Anthony Martial kuwahakikishia United ushindi.

City kwa sasa wanashikilia nafasi ya tatu wakiwa na pointi 32.

 Arsenal kwa upande wao wameweza kuonyesha kuwa bado wapo katika shindano ya kumaliza nne bora katika ligi hiyo ya Uingereza hii ni baada ya kuambulia ushindi ya mabao 3-1 dhidi ya Westham wikendi iliyopita.

Arsenal kwa sasa wapo katika nafasi ya tisa wakiwa na pointi 22.

Nani ataibuka mshindi? Yote hayo yatathibitishwa leo.

Mechi zingine zitakazochezwa leo ni;

Manchester United vs Everton

Wolves vs Tottenham