''Ati nina mimba?'' Betty Kyallo afunguka kuhusu uja uzito

Kidosho Betty Kyallo alifunguka mwanzo mwisho kuhusu madai ya kuwa na uja uzito.
Binti huyu alishikwa na mshangao sana baada ya kuona ujumbe uliokuwa ukisambaa kwenye mitandao ya kijamii na kusema kuwa hana mimba na anachotarajia kupata ni wakati mzuri tu wala si mimba.

 
''Ati I hear I’m expectant... Woi. I’m only expecting a good time tonight.” Betty alisema.

Mashabiki wengi wa mtandao wa kijamii wa Instagram walimpongeza Betty baada ya binti huyu kuweka picha kwenye mtandao wa kijamii na kuonekana ni kama ana uja uzito.
Wengi wanatumai kuwa huenda binti huyu ana uja uzito wa mpenzi wake wa sasa.

Hata hivyo, Betty alifunguka kwenye mtandao wa Instagram na kusema kuwa, hata mtoto wake, Ivanna, hawezi kubali  mama yake ajifungue mtoto mwengine.
 “Na hata Ivanna hawezi kubali.'' Betty aliandika.