Baadhi ya maneno Massawe huyatumia hewani na maana yake

massawejapanni
massawejapanni
Utangazaji wa redio ni mojawapo ya sanaa duniani zinazohitaji ubunifu mkubwa na ukakamavu wa kuwashika na kuwagandisha wasikilizaji katika spika za redio zao.

Sanaa yoyote lazima msanii achombeze maneno matamu yanayofanya kazi yake ionekane bora na ya kuvutia zaidi.

Soma hapa:

Mwimbaji wa nyimbo za mapenzi atapenda sana kuchonga mistari inayokwenda freshi na maudhui na lengo anayokusudia kwa mashabiki wa jinsia tofauti. Hali kadhalika anapofanya maonyesho jukwaani atakuwa na baadhi ya maneno kinywani ambayo wafuasi wake humtambua nayo.

Mtangazaji Massawe hajaachwa nyuma katika mtindo huu na kuna baadhi ya maneno anayoyatumia katika kipindi chake cha Bustani la massawe ili kuvutia mashabiki.

Pata uhondo hapa:

Tumekusogezea hapa baadhi ya tungo virai (phrases) anazopenda kutumia:

  1. "Nafurahi kuwa tupo pamoja nawe"

Baada ya nyimbo inayocheza hewani kumalizika, mtangazaji huyu anapenda sana kuanza na maneno haya kama kitambulisho cha kufungua shoo.

     2. "Ngwenee"

Hili ni tamko ambalo lina asili ya lugha ya Kikamba na huwa na maana ya ‘Nakuona’. Kwa haraka haraka unaweza toa ubashiri wako na kusema kuwa Massawe husema hivi labda kwa sababu anatoka maeneo ya ukambani au labda ni mbinu ya kugeuza ndimi na kuwavuta wasikilizaji kutoka jamii hiyo.

    3 ." Uko hii town? Au niko hii town au labda hii ni town"

Massawe hutumia maneno haya mara kwa mara. Staa huyu huwa anataka kujua mashabiki wake wanategea kipindi wakiwa maeneo gani.

Soma pia: