Vitendo vya baadhi yao hata hivyo vimetilia doa ukweli wao na hata hadhi zao hasa machoni pa watu .Kinachoshangaza hata hivyo ni kwamba licha ya mkinzano wa vitendo na mahubiri yao ,bado wanaaminika sana na wafuasi wao ambao huwatetea na kuwafuta kote . Kuna baadhi ya watu hasa wanawake ambao huamini na kuogopa kila wanachoambia na wahubiri wao.Kuna visa ambavyo vinajulikana vya watu kungoja wataoana lini au ahata kuoa nani watakapoambiwa na mhubiri wao! Hii hapa orodha ya baadhi ya wahubiri wazushi na wanaojulikana kwa sababu moja au nyingine –nzuri au mbaya .
5.Victor Kanyari aka Bishop Mwangi
Pastor Kanyari anajulikana sana kwa miujiuza yake ‘feki’ na hata alijipata pabaya wakati makala maalum ya runinga yalipomuangazia akifanya utapeli wake .Pia amefahamika sana kwa wito na ombilake la sadaka ya shilingi 310. Baada ya kuvurugika kwa sifa na jina lake .aliamua kubadilisha jina lake na sasa anafahamika kama Bishop Mwangi . Chini ya jina jipya na sifa tofauti siku hizo anaitisha sadaka ya shilingi 250 .wakati alipokuwa katika kilele cha utapeli wake ,alifanya miujiza yake kutumia kemikali ya potassium permanganate, iliyokuwa ikgeuka rangi kuwa ya zambarau inapowekwa majini .