Kupitia ujumbe wa Twitter ,Owino amesema wakenya wanafaa kujitokeza kwa wingi ili kuunga mkono kura ya maoni na kumaliza migogoro ya kila wakati wa uchaguzi .Babu ni mfuasi mkubwa wa Raila na amekuwa akikabiliana vikali na wote wanaompinga waziri mkuu huyo wa zamani . Ingawaje Odinga hajatangaza nia ya kugombea urais mwaka wa 2022 , washirika wake wa karibu kama Babu wanaamini kwamba ndiye mgombeaji mkuu katika kipute hicho .
We must change the constitution and Raila MUST be the PRESIDENT in 2022.Kenyans must prepare for a Referendum to avoid loss of lives and destruction of properties after elections.
— Babu Owino (@HEBabuOwino)
Matamshi kama hayo yamewahi kutolewa na Seneta wa Siaya James Orengo na kakake Raila Oburu Odinga .
Baadhi ya viongozi walio katika mrengo wa naibu wa rais William Ruto anayelenga kumrithi rais Uhuru kenyatta wamekuwa wakimshtumu Odinga kwa kuendeleza ajenda ya kurekebishwa katiba ili kujitengezea wadhifa wa uongozi serikalini.