Watalii sita akiwemo mwanamke mmoja wa ufaransa wamekamatwa huko Peru kwa kwenda haja kubwa katika hekalu moja linaloitumiwa kama makazi ya utamaduni wa taifa hilo ya Machu Picchu." watalii hao sita wamezuiliwa na wanachunguzwa na maamlaka husika kwa uhalifu huo dhdi ya makazi ya kiutamaduni’ afisa mmoja wa utawala amenukuliwa akisema siku ya jumatatu .
Watalii hao walikamatwa siku ya jumapili baada ya maafisa wa mbuga na polisi kuwapata katika eneo ambalo hawakufaa kuwepo kwenye hekalu hilo kwa jina ‘Temple of the Sun’. Wanakabiliwa na adhabu ya hadi miaka mine jela endapo watapatikana na hatia kwa kutilia doa urithi na utamduni wa Peru .
Eneo hilo la makavazi liligunduliwa mwaka wa 1911 na raia wa Marekani Hiram Bingham. UNESCO ililitaja kama eneo maalum la utamaduni linalofaa kulindwa mwaka wa 1983 .