Bonge la Hit! Harmonize arejea na wimbo mpya ''Bed Room''

NA NICKSON TOSI

Masaa machache tu baada ya kujikuta pabaya baada ya nyimbo zake alizokuwa ameziweka kwenye mitandao ya Youtube kuondolewa kwa madai ya kuiba beats.Msanii huyo amerejea na wimbo mwengine mpya wa Bed Room ambao katika mtandao wa Youtube umefikisha ufuasi wa watu takriban 92,337 ambao washaufwatilia .

Albamu yake iliyokuwa imeondolewa kwenye Youtube ilikuwa na nyimbo 18 ambazo zilikuwa zinafanya vizuri kabla ya kupoteza ufuasi baada ya kuondolewa youtube.

Ametoa wimbo baada ya wasanii kama Rayvanny kutoa wimbo kuhusiana  na Corona ambao umekuwa ukifanya vyema katika mitandao ya kijamii.