BREAKING NEWS: MKASA: Watu 5 wa familia moja wafariki Mwatate

  Watu watano wamefariki  katika eneo la  Kighombo huko  Mwatate mkaunti ya Taita Taveta baada ya maporomoko ya ardhi  kuivunika nyumba yao kufuatia mvua kubwa inayonyesha katika eneo hilo . Waliofariki ni  Mwanamme mmoja ,mkewe na watoto wao watatu . Miili ya mwanamme huyo,mkewe na mtoto mmoja imepatikana huku juhudi za  kuitafuta miili miwili ya watoto wao wengine ikiendelea .

Kamishna wa kaunti hiyo Rhoda Onyancha  amewatahadharisha wakaazi wa Voi na sehemu nyingine zilizo katika hatari ya kukumbwa na maporomoko ya ardhi kuhamia maeneo  yenye miinuko yaliyo salama .