- Orodha ya watu mashuhuri ambao walifunga pingu za maisha 2020
Licha ya mwaka wa 2020 kuwa mgumu kwa baadhi ya wakenya na hata wengi kuathirika kikazi na kupoteza kazi zao kuna wale walissema mioyoni mwao kwamba hawatamaliza mwaka huu bila kusema 'yes i do'.
Kuna baadhi ya watu mashuhuri ambao waliunga pingu za maisha mwaka huu na hii hapa orodha hiyo;
1.Pascal Tokodi na Grace Ekirapa
Wawili hao walifunga ndoa ambayo ilikuwa siri, kwa wanamitandao huku,wengi wakielewa kwamba haikua harusi mbali ilikuwa video ya wimbo.
Hivi majuzi wawili hao walithibitisha kwamba ni wapenzi kupitia kwenye mitandao yao ya kijamii ya instagram.
Wawili hao walifunga ndoa mnamo Octoba.
2.Anerlisa Muigai na Ben Pol
Picha za hafla hiyo zilienea kwenye mitandao ya kijamii Octoba huku zikithibitisha kwamba wawili hao wamefunga pingu za maisha.
3.Khula Budi
Muigizaji wa kipindi cha Maria alioa mpenzi wake mwaka huu, Agosti huku hafla hiyo wengi wakiitambua kuwa hayuko kwenye 'market' kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram.
4.Nyong'o Junior
Mwanawe gavana wa Kisumu Anyang Nyong'o alioa mpenzi wake Wanja Wahoro Julai mwaka wa 2020.
5.Esma Platnumz
Esma alifunga pingu za maisha na mumewe mwezi wa sita mwaka huu huku, tarehe 39 Julai wakiweka sherehe ya kipekee aliohudhuriwa na baadhi ya wasanii wa lebo ya WCB.
6.Queen Darleen
Dada yyake staa wa bongo Diamond aliolewa na mpenzi wake Mtoro, na kuwa mke wa pili.