TANZIA: Mamake mbunge wa Kibra Imran Okoth ameaga dunia

Ajwang'
Ajwang'

Mama mzazi wa Mbunge wa Kibra Imran Okoth, Angeline Ajwang ' ameaga dunia.

Aliaga Jumamosi asubuhi.

Akiandika kwenye mtandao wake wa Twitter, Imran aliandika,

"Katika uhai wako, tulikupenda sana, katika kifo bado tunakupenda. Unashikilia nafasi katika mioyo yetu, nililia sana wakati uliaga lakini naahidi, sitaacha machozi yafunike tabasamu ambalo umenipa wakati ulikuwa hai. Najua unasikiliza kutoka juu. Kwaheri mama. "

 

Imran alichukua nafasi kutoka kwa kaka yake, Ken Okoth ambaye aliaga dunia baada ya kuugua  saratani mnamo 2019.

Ken, ambaye alikuwa na miaka 41, alikuwa akihudumia muhula wake wa pili. Ajwang 'alikuwa amepinga uteketezwaji wa Ken, ingawa mwishowe ulifanyika.

Alitaka mtoto wake azikwe Homa Bay.