Sijawahi elewa kwa nini mimba yangu ilitoka mapema-Mpenzi wake Mulamwah

Muhtasari
  • Mpenzi wake Mulamwah asema hajawahi elewa kwanini mimba yake ilitoka mapema
  • Caroline alisema kwamba mshabiki wengi walimkejeli ni kama alikuwa na chaguo la mimba yake itoke
  • Pia alisema kwamba wengi walisema kuwa wengi walisema kwamba alitoa mimba kwa hihari yake ambapo ni uongo

Caroline Muthoni mpenzi wake Mulamwah akiwa kwenye mahojiano na Radiojambo alisema kwamba wanamitandao wengi walimkejeli sana baada ya mimba yake kutoka mapema.

Muthoni mwaka jana mimba yake ilitoka mapema, huku akisema kwamba hajui sababu ya mimba yake kutoka.

"Hadi leo sijawahi elewa kwanini mimba yangu ilitoka mapema, madaktari waliniambia kwamba nilikuwa na dhiki na ilisababisha mimba yangu kutoka

 
 

Nilipokea kejeli nyingi kutoka kwa mashabiki, wengi walikuwa wananiuliza kwanini nilikubali mimba ya Mulamwah ikatoka, ni kama nilikuwa na chaguo

Mulamwah alinipa ushauri baada ya mimba yangu kutoka mapema,mimi naogopa sana kupta ujauzito kwa sababu ya yae yalitokea,"

Caroline na Mulamwah wamekuwa katika uhusiano wa kimapenzi kwa miaka 4.