(+Video)Kwa sasa niko 'single' sina mpenzi,'msanii Nicha the Queen asema

Muhtasari
  • Nicah the Queen asema hana mpenzi yuko 'single' huku akisema atarejea kwenye tasnia ya muziki
Nicah the Queen
Image: Studio

Msanii Nicah the Queen akiwa katika mahojiano na radiojambo aliweka mambo wazi na kusema kwamba mchekeshaji Ofweneke ni baba mzuri sana licha ya wao kutengana.

Huku akizungumzia umaarufu wake Nicha alisema, kuwa baba wa watoto wake hakufanya afahamike mitandaoni.

"Ofweneke hakufanya nifahamike sana kwenye mitandao ya kijamii, amekuwa baba mzuri kwa watoto wangu

 

Niliachana na aliyekuwa mpenzi wangu kwa ajili tulikuwa mbali, sana sana hangeelewa kamba mimi ni mama ananiita tunaenda kujivinjari lakini wakati huyo mimi nawasaidia watoto wangu kufanya kazi ya ziada

Kwa sasa sioni mtu niko single lakini akija ni sawa asipokuja tunangoja kutoka kwa Mungu," Alisema Nicah.

Nicah alifichua kwamba mwaka huu atarejea kwenye tasnia ya muziki.

"Sikuwa nimeacha muziki lakini nitarejea mwaka huu, baada ya uhusiano wangu kukamilika nilikuwa napitia mambo mengi sana

Kama mwanamke kuwa katika tasnia ya burudani si rahisi sana,"

Hii hapa video ya mahojiano yote;

Radio Jambo Kenya | Ongea Usikike | Ni kituo nambari moja Kenya kwa matangazo ya kiswahili. Vipindi vyake vina jumuisha Spoti,Mijadala moto moto na muziki wa Kiafrika #RadioJamboKenya Subscribe to RadioJambo Youtube - https://bit.ly/39wwc6u Mitandao ya Kijamii Instagram - https://rb.gy/e154d1 Facebook - https://rb.gy/09d1b9 Twitter - https://rb.gy/e23220