Jipende mwenyewe kabla ya kumpenda mtu mwingine yeyote-Corazon Kwamboka

Muhtasari
  • Corazon awashauri mashabiki wake wajipende kwanza kabla ya kumpenda mtu mwingine yeyote
corazon
corazon

Mwanasosholaiti Corazon Kwamboka kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram aliweka wazi kwamba katika maisha yake ya mapema alipokuwa katika  miaka yake ya 20 hakuamini kwamba angeweza kukaa bila mpenzi.

Huku akiwashauri mashabiki wake pia aliwambia kwamba wanapaswa kujipenda kwanza kabla ya kumpenda mtu mwingine yeyote.

Pia alifichua kwamba alipatana na watu bandia huku akiingia katika mahusiano ya kimapenzi ambayo yalimuumiza roho.

 

Jipende mwenyewe kabla ya kumpenda mtu mwingine yeyote, kwa sababu huyo ndiye utakayetumia maisha yako yote.

"Katika miaka yangu ya mapema ya 20 sikuwahi kuamini Katika kuwa mseja, kutumia wakati na mimi mwenyewe au hata kwamba ninaweza kuwa kamili bila kundi la rafiki au rafiki wa kiume. Kwa hivyo nilishirikiana na watumiaji  mitandao na watu bandia nanikajihusisha na wanaume ambao ni sumu na nikakaa muda mrefu kuliko vile ningepaswa kuwa tu kwa sababu ya uchumba, hakuna maana, kusudi au siku zijazo." Aliandika Corazon.

Corazon amesema ilimchukuwa muda mrefu kuwaachili watu bandia ambao walikuwa katika maisha yake na kukaa peke yake.

"Ilichukua kukomaa kugundua kuwa ilinibidi niachane na watu wote wenye sumu maishani mwangu, kuwa peke yangu kwa muda na kugundua fikra wa kweli aliye ndani, sasa ninajitosheleza zaidi

Ninapenda marafiki kuwa na mtu wa kubembeleza na kumpenda ni jambo la kupendeza lakini sio kila kitu na haipaswi kuwa. Nakupenda kwa kweli."