- Wanawake mashuhuri waliopata matatizo ya ujauzito
- Kwa kweli wanawake wengi hupitia safari ndefu baada ya kugundua kwamba ni wajawazito
Ni matamanio ya kila mwanamke kuitwa mama, na kutaka kujifungua vyema na mtoto mwenye afya endapo ni mjamzito.
Kwa kweli wanawake wengi hupitia safari ndefu baada ya kugundua kwamba ni wajawazito.
Ni safari ambayo inahitaji uvumilivu na furaha kia wakati, kuna baadhi ya wanawake mashuhuri humu nchini ambao wana ushuhuda wa kutosha kuhusu safari yao ya ujauzito hadi mahali walijifungua.
Wanawake hao wamekuwa mfano mwema kwa mashabiki na wanawake ambao wamekata tamaa ya kupata ujauzito.
Wanawake hao ndio hawa hapa;
Size 8
Msanii huyo wa nyimbo za injili ana ushuhuda mwema changamoto ambazo alipitia akiwa mjamzito na hata baada ya kujifungua mwanawe wa pili.
Kambua
Msanii Kambua alipokea kejeli nyingi baada ya kukaa sana bila ya kupata ujauzito, bali na hayo Mungu aliwanyamazisha maadui wake kwa kumbariki na mtoto.
Bridget Achieng
Mwanasosholaiti huyo ni wa kupigiwa mfano hata baada ya kujifungua, amekuwa akimlea mwanawe kwa njia ya kipekee na hata kujitia nguvu kila kuchao.
Avril
Ni msanii ambaye anapendwa kwa sana na mashabiki wake, vril amebarikiwa na mtoto mmoja, ambapo uvumi ulitokea kamba alifanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua
Akiwa kwenye mahojiano na radiojambo msanii huyo alifutilia mbali madai hayo na kusema kwamba alijifungua kawaida licha ya kupata changamoto nyingi.
Janet Mbugua
Mwanahabari huyo wa zamani wa runiga ya Citizen ni mwenye ujasiri wa kipekee, ata baada ya kupitia changamoto wakai wa ujauzito wake.