Huku Wakenya wengi wakiamini kuwa Hamo alichujwa kwa upotovu wa nidhamu, baadhi ya wandani wake wamekanusha madai hayo wengine wakitangaza kuwa alijiuzulu mwenyewe kwa sababu zake binafsi.
Hatima ya kazi yake mcheshi tajika Profesa Hamo kwenye kampuni ya Royal Media Services imezua gumzo mitandaoni.
Hii ni baada ya mtangazaji kutosikika hewani kwa kipindi cha takriban wiki mbili zilizopita. Hakuna tangazo lolote rasmi lililotolewa na mtangazaji huyo au kampuni ya RMS kuhusu kilichomtokea Hamo ambaye amekuwa akishirikiana na mwanahabari Jeff Koinange kwenye kipindi ‘Morning Drive’ kwenye redio ya Hot 96 tangu mwaka wa 2018.
Hata hivyo, nduru za kuaminika zinaarifu kuwa mcheshi huyo wa Churchill si mwajiriwa wa RMS tena. Wengi mtandaoni wamehusisha masaibu hayo ya Hamo na mgogoro uliotokea baina yake na mcheshi mwenzake alamaarufu kama ‘Jemutai’
Awali Jemutai alimkashifu Hamo kwa kuwa baba mpotevu. Wawili hao wamezaa watoto wawili pamoja nje ya ndoa ila zogo lilivuma Jemutai alipoweka wazi mtandaoni kuwa amekuwa akishughulikia watoto wale peke yake. Alimtaka Hamo kuwajibika zaidi kwenye jukumu la kulea wana wale.
Zogo hilo lilimchochea Hamo kutaka wawili hao kufanya kipimo cha DNA ili kubaini kuwa kweli wana wale wawili ni wake kweli. Matokeo ya kipimo hicho yalitokea mwanzoni wa wiki na kutangazwa naye Jemutai kupitia kurasa zake za mtandao. Hamo hata hivyo amebaki kimya akionekana kutotaka kuzungumzia swala hilo.
Huku Wakenya wengi wakiamini kuwa Hamo alichujwa kwa upotovu wa nidhamu, baadhi ya wandani wake wamekanusha madai hayo wengine wakitangaza kuwa alijiuzulu mwenyewe kwa sababu zake binafsi.
“Pofesa Hamo hakuchujwa RMS” aliyekuwa mtangazaji wa Hot 96 na Radio Jambo aliandika kwenye mtandao wa Twitter.
he wasn't fired
— Annitah Raey (@AnnitahRaey) May 12, 2021
Kufikia sasa, Hamo hajatoa tangazo lolote kuhusu hatima yake