•Sonko adai kuwa tendo la wanawake kuwa na bwana zaidi ya mmoja linafanyika nchini ingawa bado halijakubalika.
•Asema pia kuwa mwanaume hawezi muacha mke waliyezaa na kuvumilia shida naye kwa sababu ya mpango wa kando
Aliyekuwa gavana wa kaunti ya Nairobi ambaye alitimuliwa,Mike Sonko Mbuvi ameonekana kupendezwa na hatua ya serikali ya Afrika Kusini kuwaruhusu wanawake kuwa na mabwana wengi.
Kupitia jumbe alizochapisha kwenye mitandao yake ya kijamii, Sonko amedai kuwa hivi karibuni wanawake wa Kenya wataruhusiwa kuwa na bwana zaidi ya mmoja. Amesema kuwa hatua ile itakuwa haki kwani mabibi wa mabwana ambao wana wapenzi wengi watakuwa wanalipisha kisasi.
Polyandry is already being practiced in Kenya as South African Government also proposes the same to be passed. Our wives will soon be allowed to marry other men. It will become a tit for tat fair game kwa mabibi wa team mafisi wafeel vile their hubbies feel wakiwahanya. pic.twitter.com/NamFieT1S2
— Mike Sonko (@MikeSonko) May 18, 2021
“Hapo nawaunga mkono wanawake. Je wewe fisi unakubali bibi yako aolewe tena na mwanaume mwingine ukiwa nae” Sonko aliandika.
Kwa upande mwingine, Sonko pia amesema kuwa mwanaume hawezi kumuacha bibi aliyepata watoto na kuvumilia shida naye kwa miaka mingikwa sababu ya mpango wa kando.
In my opinion a man can't divorce his wife who's the mother of his children & whom they've suffered together for many years for a sidechick or a 2nd wife. He better keep both of them as 1st and 2nd wife or sidechick etc. and on top of that give maximum respect to the 1st wife.
— Mike Sonko (@MikeSonko) May 18, 2021
"Ni heri awaoe wote wawili kama bibi wa kwanza na wa pili. Jambo hilo linampa heshima mke wa kwanza" Sonko alidai