'Shukrani,'Kambua Atoa kibao kipya Baada ya Kumpoteza mwanawe

Muhtasari
  • Kambua Atoa kibao kipya Baada ya Kumpoteza mwanawe

Msanii wa nyimbo za injili na mtangazaji maarufu Kambua, alirejea mitandaoni  siku ya Ijumaa baada ya kuchukua likizo kwa miezi mitatu.

Aliwashukuru mashabiki wake kwa kumuombea alipopitia magumu, bali na hayo hakuwashukuru mashabiki bali alitoa kibao cha shukrani kwa Mungu.

Kambua amesema wimbo huo mpya ameotoa wakati wa dhiki na faraja kwa wakati mmoja.

" Shukrani ni wimbo ambao niliotoa wakati wa huzuni mwingi ila pia kwa shukrani kwa Mungu wangu

Hali hizi mbili kwa sasa zinaambatana na najua Mungu anabaki kuwa Mungu kwa kila ambacho ametufanyia

Mungu huwa anatufaruji na kutuahidi kutembea nasi katika bonde la mauti, kwa hivyo, anaponiunua na kunifariji, hebu na pia akutendee pia wewe, Mungu anajua kuwafidia wanawe, najua hawezi kukuacha, Mungu ni mkuu," Kambua Alisema.

Mashabiki walimkaribsha msanii huyo, kwa furaha huku wengi wakikiri walikuwa wamempeza sana.