Sijawahi elewa kwanini huwa napendeza wanaume ambao wameoa-Muigizaji Sandra Dacha

Muhtasari
  • Sandra Dacha afichua haya kuhusu maisha yake
  • Muigizaji Sandra Dacha ambaye alifahamika sana kupitia kwenye kipindi cha Auntie, ni miongoni mwa wasanii ambao wanaendelea kutia bidii kwenye tasnia ya burudani
Sandra Dacha
Image: HIsani

Muigizaji Sandra Dacha ambaye alifahamika sana kupitia kwenye kipindi cha Auntie, ni miongoni mwa wasanii ambao wanaendelea kutia bidii kwenye tasnia ya burudani.

Sandra amekuwa akiwapa mashabiki wake hasa wenye mwili mkubwa, ambao hukejeliwa sana na wanamitandao motisha ya kujipenda jinsi walivyo.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa facebook muigizaji huyo aliwauliza wanaume ambao hawana wapenzi kwanini huwa wanamuogopa.

"Sijawahi elewa sababu kwanini huwa napendeza wanaume ambao wameoa,Single men mbona huwa mnaniogopa? Ama ni clutch ya gari KUBWA ndio hamjui mahali inapatikana🤣😂🤣," Aliandika Sandra.

Hizi hapa baadhi ya hisia za mashabiki;

Mc Charlie Comedian: Ata loli iwe kubwa ajy ..nafasi ya dereva ni ile ile😊

Osomba Fredrick: Omera nyako!!!!trackter inataka experience if not a very serious accident will happen ahead with no single life saved

Waithira Cecilia: I love your confidence 💯✔️

Fred Lumumba: We ukiangalia tu hivi unaona ukitoshea bafu ya bedsitter 😂😂😂

Nelly Waeni: Experience watoe wapi ?🤣