- Muigizaji Njambi afunguka kuhusu kuharibika kwa mimba yake
- Muigizaji wa kipindi cha Real house of Kawangware Njambi, akiwa kwenye uhusiano alifunguka uhusu kuharibika kwa mimba yake mnamo mwaka wa 2018
Muigizaji wa kipindi cha Real house of Kawangware Njambi, akiwa kwenye uhusiano alifunguka uhusu kuharibika kwa mimba yake mnamo mwaka wa 2018.
Kulingana na Njambi alipoteza matumaini na imani yake kutoka kwa Mungu baada ya mimba yake kuharibika mapema kwani alikuwa anapitia changamoto nyingi.
"Kuharibika kwa mimba kuliniathiri kihemko, kiakili, kiroho na kimwili
Hakuna hasara bora ikiwa ni kuzaa mtoto mchanga au kuharibika kwa mimba maumivu ni sawa.
Nilipoteza mimba kwa miezi 5.Tulikuwa tumeenda mahali pengine na marafiki zangu wakati tulikuwa kwenye matatu nilikuwa najisikia vibaya
Nilihisi kama kupiga pumzi, jasho kati ya mambo mengine.Niliwaambia marafiki zangu kwamba nilihitaji kwenda kwenye chumba ha kujisaidia hapo ndipo niliona navuja damu " Njambi alieleza.
Njambi anasema ingawa alikuwa amepoteza kuona wanawake wengine wakishindwa na huzuni walimvunja moyo.
"Kisha nikapelekwa kwenye wadi ambayo mama walikuwa wamepoteza watoto wao,Sehemu ya kusikitisha zaidi ni mwanamke ambaye alikuwa amepoteza mtoto wake akawa dhaifu kiakili
Hakuweza hata kwenda kwenye chumba cha kujisaidia, kwa bahati nzuri mama alikuwepo kumsaidia.
Baada ya kutoka hospitalini niligundua walikuwa wameacha kondo la nyuma mwilini mwangu.
Nilikuwa na maumivu sana, kwa hivyo tulirudi hospitalini kwa hivyo ilinibidi 'kusafishwa.' Kuharibika kwa mimba kulivunja urafiki na mahusiano yangu
Sikujua nitazungumza na nani, nilishughulikia peke yangu na iliathiri uhusiano wangu na baba yangu mchanga
Hasara ilituvunja kwani yeye pia hakujua jinsi ya kuhuzunika,Katika kipindi hicho nilipoteza hali yangu ya kiroho na imani yangu kwa Mungu, sikuwa na kazi.
Mnamo mwaka wa 2019 nilibarikiwa kupata mtoto wa kiume. "Alisema Njambi