Siwezi ngoja kusherehekea nawe Jumamosi,'Ujumbe wake Diamond kwa mwanawe Tiffah anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa

Muhtasari
  • Wawili hao walibarikiwa na mtoto mwingine, Nillan Dangote
    Diamond ameonekana kuwa karibu na watoto wake wawili, ikilinganishwa na wale wengine wawili.
  • Hivi karibuni Diamond alikuwa nchini Afrika Kusini, ambapo alijiunga na watoto wake
  • Pia tumemuona Tiffah akiwa na upendo wa kipekee kwa baba yake
Tiffah Dangote
Image: Instagram

Ni furaha ya kila mzazi kumuona mwanawe akikua, akiwa na afya na kupokea elimu bora, Diamond ni miongoni mwa wasanii ambao wamebarikiwa na watoto wenye urembo wa kipekee.

Ingawa yeye ni baba wa watoto wanne, Diamond amebarikiwa na binti mmoja tu, Latiffah Dangote. Diamond alimpata Tiffah wakati alikuwa kwenye uhusiano na mwanasosholaiti na mfanyibiashara Zari Hassan.

Wawili hao walibarikiwa na mtoto mwingine, Nillan Dangote.

Diamond ameonekana kuwa karibu na watoto wake wawili, ikilinganishwa na wale wengine wawili. 

Hivi karibuni Diamond alikuwa nchini Afrika Kusini, ambapo alijiunga na watoto wake.

Pia tumemuona Tiffah akiwa na upendo wa kipekee kwa baba yake.

Anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa Diamond alifichua kwamba atakuwa naye JUmamosi hii, ili kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Huu hapa ujumbe wake;

Heri ya kuzaliwa binti yangu mzuri na mzuri lovely @princess_tiffah πŸ’ .... maneno hayawezi kuelezea jinsi ninavyokupenda Miss WorldπŸ‘Έ .... siwezi subiri kusherehekea siku hii ya kuzaliwa na wewe, Jumamosi hii .... β€πŸŽ‚β€ @princess_tiffah β€πŸŽ‚β€," Aliandika Diamond.

Hizi hapa jumbe za mashabiki;

akotheethebosslady: Happy Birthday princess

mbaureloadedVerified: Happy birthday πŸŽ‚ πŸ‘‘ princess ❀️

amjosephinegold: Hbd baby girls 😍😍 🎁 more life

the_only_boss_on_this_: Happy birthday to you beautiful

prettahnellie254: Hbd tee