Nilipoteza imani yangu kwa Mungu baada ya kuachwa na mpenzi wangu mara 2-Kipusa asimulia

Muhtasari
  • Kuna baadhi ya changamoto ambazo watu wengi hupitia na kukata tamaa huku wengi wakiamua kutoa muamini Mungu
  • Nikiwa katika ziara yangu nilikutana na kipusa ambaye alinisimulia  masaibu ambayo alipitia kwenye maisha yake ya mapenzi
sad woman
sad woman

Kuna baadhi ya changamoto ambazo watu wengi hupitia na kukata tamaa huku wengi wakiamua kutoa muamini Mungu.

Sio mmoja au wawili bali asilimia kubwa ya watu wamekuwa wakikiri kwamba waliacha kumuamini Mungu kwa jambo moja au lingine.

Nikiwa katika ziara yangu nilikutana na kipusa ambaye alinisimulia  masaibu ambayo alipitia kwenye maisha yake ya mapenzi.

KUlingana na kipusa huyo mpenzi wake alimuacha kwa mara ya kwanza, lakini akamrudia punde tu alipomuamini Mungu.

Huu hapa usimulizi wake;

"Katika maisha ya kupenda sijakuwa na bahati, kwani moyo wangu umejawa na uchungu mwingi, nilikuwa na huyu mwanamume ambaye tulikuwa tunapendana sana

Tulichumbiana kwa miaka miwili, mapema mwaka huu  aliniambia kwamba tunapaswa kuachana kwani mimi sio ubavu wake, sikupinga lolote tuliachana kwa roho moja

Nilimuomba Mungu anifungulie nja na aweze kumrudisha mpenzi wangu kwani sikuwa tayari kumpenda mwanamume mwingine, ndio Mungu alijibu maombi yangu na imani yangu iliongezeka kwake

Miezi chache iliyopita aliniacha na kumwendea mwanamke mwingine, na hamna makosa mabayo nilitenda wala kumfanyia chochote

Kuanzia wakati ainiacha nilipoteza imani yangu kwa Mungu kwani sina furaha kamwe."

Je ni ushauri upi unapaswa kumpa mwanamke huyu, je azidi kumsubiria mpenzi wake au aendelee na maisha yake na kumrudia Mungu?