Mbinu maarufu ambazo wasanii wa Kenya hutumia kutafuta kiki

Muhtasari

•Kwa lugha ya mtaani, kiki (clout) ni kitendo cha mtu haswa msanii kuanzisha drama ili kuibua gumzo ama kutaka kuangaziwa zaidi na watu.

Image: INSTAGRAM// WILLY PAUL

Je wafahamu kiki ni nini?

Kulingana na Kamusi ya Kiswahili, neno kiki linamaanisha pigo la mpira kwa kutumia mguu.

Kwa lugha ya mtaani, kiki (clout) ni kitendo cha mtu haswa msanii kuanzisha drama ili kuibua gumzo ama kutaka kuangaziwa zaidi na watu.

Wasanii wengi, sio tu nchini Kenya bali kote dunia wanajulikana kutafuta kiki sana haswa wanapotazamia kutoa wimbo mpya ama kufanya tamasha.fulani.

Kunazo mbinu tofauti ambazo hutumika kutafuta kiki na zote hutegemea ubunifu wa anayetafuta kiki.

Hizi hapa baadhi ya mbinu za kawaida ambazo wasanii nchini Kenya wanapendelea kutumia sana:-

1. Mahusiano

Kwa kawaida ndoa ama mahusiano hufanyika kati ya wawili ambao wanapendana na wanatazamia kuanzisha familia pamoja.

Aghalabu watu wanapoamuua kujitosa kwenye mahusiano huwa wanaangaziwa sana na jamii wengi wakitaka kufuatilia mwelekeo wa mahusiano yale.

Hata hivo hapo awali mahusiano yametumika vibaya na baadhi ya wasanii ambao hujifanya kama kwamba wako kwenye mahusiano mradi tu waangaziwe na watu.

Mbinu hii imetumika sana nchini haswa wakati msanii wa kiume anatazamia kushirikiana na msanii wa kike kwenye wimbo.

Nadia Mukami aliwahi kudanganya kwamba ako kwenye mahusiano na jamaa mwenye asili ya Kihindi kisha ikafahamika baadae kuwa alitaka tu kumshirikisha kwa wimbo.

2. Utengano

Wakati kunao wasanii  ambao hujitosa kwenye mahusiano ili kuibua gumzo miongoni mwa watu, kunao wanandoa au wapenzi ambao haumua kujifanya kama kwamba wametengana almradi tu waangaziwe zaidi na watu.

Hii ni jambo la kawaida haswa miongoni mwa wapenzi mashuhuri ambao wanatazamia kufanya mradi pamoja kama vile wimbo ama video.

EMB ENTERTAINMENT PRESENTS BAHATI FEATURING DIANA MARUA (@BAHATIKENYA & @DIANA_MARUA) #BahatiKenya #MTAACHANATUU Available on all digital platforms: http://smartklix.com/smartlink/?id=5bd62793&c=y WRITTEN BY KEVIN BAHATI AUDIO: EMB/ MESESI/ TEDDY B VIDEO: YOUNG WALLACE #BahatiReality #BahatiKenya #BeingBahati #BahatiMusic Subscribe to the channel for latest updates: http://bit.ly/BAHATIKENYA Watch more: BEING BAHATI- http://bit.ly/BeingBahati Best Of Bahati Music- http://bit.ly/BestOfBahatiMusic Best Kenyan Music- http://bit.ly/BestKenyanMusic Best Gospel Music- http://bit.ly/BestGospelMusic Follow me on: Facebook: https://www.facebook.com/Bahati-1410030652584881 Instagram:https://www.instagram.com/bahatikenya/ Twitter: https://twitter.com/BahatiKenya Digital distribution and Promotion by Ziiki Media

Mfano mzuri ni wakati mwanamuziki Bahati na mpenzi wake Diana Marua walikuwa wanapanga kutoa wimbo 'mtaachana tu' pamoja walifanya wanamitandao waamini kwamba wametengana.

3. Ugonjwa/Ajali

Kunao wasanii ambao hupita mipaka na kujifanya kama kwamba ni wagonjwa ama wamehusika kwenye ajali ili tu waangaziwe na watu.

Ijapokuwa jambo hili ni la kusikitisha, kunao wasanii ambao kwa kawaida  hawajalishwi na matokeo ya matendo yao bora tu wanase umakini wa watu.

Mbinu hii ya kughadhabisha imetumika na wasanii wengi duniani.

Kuna gumzo mitandaoni kwamba ujumbe wa Willy Paul wa hivi majuzi kwenye mtandao wa Instagram ulioashiria kama kwamba amekabiliwa na msongo wa mawazo huenda ikawa ni kiki tu anatafuta kwani anatazamia kuzindua albamu yake hivi majuzi.

4. Ugomvi

Kunao wasanii ambao hujifanya kama kwamba wanazozana ili tu kuibua gumzo na kuangaziwa na mashabiki wao.

Wasanii hawa hukorofishana hadharani ama mitandaoni  ili kunasa watu kisha baada ya kufanikiwa wanafanya mradi wa sanaa pamoja.

Mfano mzuri wa hivi karibuni ni wakati Willy Paul na Size 8 walijifanya kama kwamba wanazozana kisha wakashirikiana kutoa wimbo 'Lenga' pamoja mnamo mwezi Julai.

5. Kashfa

Kashfa ni jambo la aibu lililofanyika kwa siri ambalo limefichuka.

Kashfa huenda ikawa ya kimapenzi, kingono au ikahusiana na masuala mengine ya maisha.

Kunao wasanii ambao hujifanya kama kwamba wamehusika kwenye kashfa mradi tu wapate kufahamika zaidi ama kuangaziwa na watu.

Kashfa za kawaida miongoni mwa wasanii ni zile ambazo zinahusisha mapenzi, ngono au mitindo ya maisha.