logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize: Mungu rudisha familia yangu, samahani binti yangu kwa mazingira magumu

Harmonize - Mungu irudishe familia yangu tafadhali. Samahani sana binti yangu. Bado nakumbuka nyakati zile tukiwa pamoja kama familia

image
na Davis Ojiambo

Burudani28 March 2022 - 11:31

Muhtasari


  • Harmonize - Mungu irudishe familia yangu tafadhali. Samahani sana binti yangu. Bado nakumbuka nyakati zile tukiwa pamoja kama familia
Harmonize na aliyekuwa mpenzi wake Sarah Michelotti

Je, msanii Harmonize ameingia mkondo wa kusongwa na mawazo kutokana na kutengana na familia yake kama staa wa Marekani wa hiphop Kanye West?

Maswali kama haya yametanda vichwqani mwa watu wengi ambao wanamfuatilia msanii huyo kwa ukaribu na pia kuyafuatilia matukio katika Sakata la kutalikiana baina ya Kanye West na mpenzi wake wa miaka 12, Kim Kardashian.

Harmonize wikendi iliyopita alionekana akituma ujumbe changamano kwa mpenzi wake kupitia instastories zake ambapo anasononeka pakubwa mpaka kumtaka Mungu airudishe familia yake, kwa kutumia maneno yale yale ambayo pia Kanye West aliwahi yatumia wakati mmoja akiomba Mungu kuirudisha familia yake.

“Mungu irudishe familia yangu tafadhali,” aliandika Harmonize kwenye instastories zake.

Kwa mara ya kwanza hakuna aliyejua msanii huyu alikuwa anazungumzia familia ani kutokana na kwamba amekuwa katika mahusiano mara mbili kabla ya mahusiano ya sasa.

Baadaye ilionekana kwamba Harmonize anaikosa sana familia yake na mchumba wake Muitaliano Sarah Michelotti ambaye walifanikiwa naye mtoto mmoja wa kike, Zulekha Nasra.

Katika kipande kingine Harmonize aliachilia ujumbe mzito kwa mwanawe Zulekha huku akimtaka radhi kwamba ikatokea amekufa leo bila kumwomba msamaha kwa kumweka katika mazingira magumu basi atakuwa mjinga wa kupigiwa mfano.

“Samahani sana binti yangu. Nitakuwa mtu mjinga sana kama nitakufa leo bila kusema samahani kwa kukuweka katika mazingira magumu, haswa kutokana na umri wako ulivyo mdogo. Ninahisi vibaya sana haswa nikiwa baba wa mabinti na singependa kuingia ndani sana kwa sababu inauma. Ila zidi kujua tu kwamba nakupenda sana, endelea kumfanya mamako kujivunia. Bado nakumbuka nyakati zile tukiwa pamoja kama familia, najivunia sana kwa mtu ambaye unakua kukuwa. Mungu akulinde, ila samahani sana,” aliandika Harmonize


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved