'Lala salama,'Wema Sepetu amuomboleza msanii maunda

Muhtasari
  • Muigizaji wa Tanzania na mrembo Wema sepetu amemuomboleza msanii Maunda Zzoro ambaye aliaga dunia katika ajali mbaya ya barabarani siku ya Alhamisi
wema 5 (1)
wema 5 (1)
Image: HISANI

Kifo ndio mwisho wa kila nafsi duniani. Wakati watu wanaondoka ulimwenguni kwa sababu moja au nyingine huwa ni wakati wa kukatisha tamaa kwa wapendwa wao.

Kila mtu anatamani kwamba kifo kingeepukika lakini ni hukumu ya Mwanadamu. Hakuna mtu anayeweza kuikwepa hata jinsi ilivyo chungu.

Muigizaji wa Tanzania na mrembo Wema sepetu amemuomboleza msanii Maunda Zzoro ambaye aliaga dunia katika ajali mbaya ya barabarani siku ya Alhamisi.

Marehemu Maunda Zzoro amekuwa mmoja wa wanamuziki wa kike nchini Tanzania ambao wamekuwa kichocheo kikubwa katika tasnia ya muziki.

"Daaaaaah.... Umeniuma Maunda....!!! Such a sweet soul.... Dada mzuri mwenye roho nzuri.... Rest in Peace babe.... Njia yetu sote.....πŸ₯²πŸ₯²πŸ₯² Condolences to your Family...πŸ™πŸΌπŸ™πŸΌπŸ™πŸΌ," Wema Aliomboleza.

Taifa linaomboleza baada ya kakake Banana Zzoro kuwa mtu wa kwanza kuthibitisha kwamba hakika dada yake ameaga dunia.

Alisema kuwa ni pigo kubwa kwa nchi nzima kwani kifo cha  Maunda kilivunja matumaini na matarajio yote waliyokuwa nayo katika Maisha yake.