logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diana Marua azidiwa na hisia baada ya kuchumbiwa na Bahati, watangaza tarehe ya harusi yao

Huku akibubujikwa na machozi, Diana Marua alijibu, "Ndiyo. Nakupenda sana na nasema ndiyo mara milioni. Na asante."

image
na SAMUEL MAINA

Burudani20 June 2023 - 04:59

Muhtasari


  • •Wakati akichukua hatua hiyo kubwa, Bahati alibainisha kuwa amekamilisha hatua zote muhimu kuelekea ndoa na sasa yuko tayari kuifanya rasmi.
  • •Kwenye ukurasa wake wa Instagram, mwanamuziki huyo alitangaza tarehe 12 Desemba kuwa siku ya harusi yao.

Mwimbaji mashuhuri wa Kenya Kelvin Kioko almaarufu Bahati alimchumbia rasmi mpenzi wake wa muda mrefu na mzazi mwenzake Diana Marua.

Wawili hao walirekodi kipindi hicho kizuri katika video iliyopeperushwa kwenye chaneli ya YouTube ya Diana Marua siku ya Jumatatu.

Wakati akichukua hatua hiyo kubwa, Bahati alibainisha kuwa amekamilisha hatua zote muhimu kuelekea ndoa na sasa yuko tayari kuifanya rasmi.

"Umenipatia moyo wako. Kusema kweli kutoka ndani ya moyo wangu, siichukulii virahisi. Kitu kimoja ambacho ninataka sana kufanya mwaka huu, nataka tu kuhakikisha nimefanya sawa, najua nimeenda kwa familia yako kwa utambulisho lakini mwaka huu nataka tufanye harusi ya kweli na nataka kukuoa," Bahati alimwambia mchumba wake.

Aliongeza, "Nataka kuhakikisha kwamba nimekuoa kiroho rasmi. Mungu anajua moyo. Nataka kuifanya kwa utamaduni. Kwa heshima ya wazazi wako, baba yako, nakuahidi kwamba mwaka huu nitakufanyia harusi kubwa na bora zaidi ambayo macho yako yamewahi kuona. Hiyo ndiyo ahadi yangu."

Pindi tu baada ya kusema maneno hayo matamu kwa Diana ambaye wakati huo tayari alikuwa amezidiwa na hisia kali, mwimbaji huyo wa zamani wa nyimbo za injili alitoa pete ambayo alikuwa ameibeba kwenye kasha dogo na kisha kumuuliza mama huyo wa watoto wake watatu iwapo ataolewa naye.

"Nataka kuchukua fursa hii kukuonyesha kwamba namaanisha hilo na nakuthamini. Ndiyo maana nataka kufanya upya viapo vyetu. Nataka kukuuliza kwa mara nyingine, "Je, utaolewa nami?" alimuuliza.

Huku akibubujikwa na machozi, Diana Marua alijibu, "Ndiyo. Nakupenda sana na nasema ndiyo mara milioni. Na asante."

Mama huyo wa watoto watatu aliendelea kububujikwa na machozi ya furaha kabla ya kueleza jinsi anavyotazamia siku hiyo kubwa katika maisha yao ambapo hatimaye watarasimisha ndoa yao.

"Najua tumekuwa tukipanga. Tumeongea kuhusu hili lakini sasa ni kweli kabisa. Itafanyika. Siwezi kusubiri kufunga pingu za maisha na kusema ndiyo mbele ya kanisa, dunia yote na mbingu. Naahidi kwamba siku zote nitajisalimisha kwako. Nakupenda sana kila siku," Diana alimwambia mpenziwe.

Kando na pete, Bahati pia alimpa mchumba wake hereni kama ishara ya uchumba.

"Ninataka kuzeeka na wewe, kusafiri ulimwengu na wewe, kusafiri ulimwengu na watoto wetu pamoja na wewe. Nitasema ndiyo kila siku. Mungu atulinde kila siku," Diana alimhakikishia mwanamuziki huyo.

Baadaye, kwenye ukurasa wake wa Instagram, mwanamuziki huyo alitangaza tarehe 12 Desemba kuwa siku ya harusi yao.

"Alisema ndiyo.  Na natangaza rasmi kwamba Desemba 12 ni siku ya harusi yetu," Bahati alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved