logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alikiba ampiga kumbo tumboni Diamond, "Mimi sijali mambo ya trend kama wewe!"

Alikiba alikuwa na mkusanyiko wa wasanii wengine akiwemo meneja wake pamoja na msanii Marioo.

image
na Davis Ojiambo

Burudani11 July 2023 - 10:34

Muhtasari


  • • Alikiba alikuwa na mkusanyiko wa wasanii wengine akiwemo meneja wake pamoja na msanii Marioo.

Wasanii wengi wa Bongo Fleva wameimezea mate sana mwezi huu wa Julai wakisema kuwa ndio mwezi wa kurudi upya kwenye muziki baada ya kupoa kwa muda.

Iianza na msanii Diamond Platnumz kutangaza kwamba mwezi Julai ndio atafanya urejeo upya kwa muziki na hata kutamba kwamba atashikilia chati kwenye trend namba moja hadi Janauri mwakani atakapochukua likizo fupi kumpisha msanii wake mpya.

Baada ya kutaja kuwa analenga kuteka trends zote za muziki, Alikiba alitoa tamko ambalo limetajwa kuwa mshale kwa kambi ya Diamond Platnumz akisema kuwa yeye hutoa miziki mikali na wala hajali mambo na trends.

Alikiba alikuwa na mkusanyiko wa wasanii wengine akiwemo meneja wake pamoja na msanii Marioo.

Katika maongezi yao ilionekana Marioo na Alikiba walikuwa wanatoa collabo na Marioo alisema kuwa noma hiyo isipohit basi ako radhi kumpa meneja wa Alikiba shilingi milioni 50 za Kitanzania.

Hapo ndipo ALikiba alidamka na kutia neno akisema kuwa;

“Nyinyi mnajali kuhusu trends,” Alikiba alisema.

Kauli hii ilipokelewa kwa njia tofauti na mashabiki wa muziki wa Bongo Flava baadhi wakisema kuwa kauli hiyo ilikuwa inalenga kwa Diamond baada ya kusema kuwa atakuwa anashikilia namba moja kwenye trends.

Kwenye sehemu ya komenti ilikopakiwa hiyo video, walionekana wakiotesha ugomvi wa wasanii hao wawili, licha ya Diamond mara nyingi tu kukanisha hadharani kwamba yeye na Kiba hamna uadui baina yao bali ni vyombo vya habari na mashabiki ambao wamekuwa wakiwapiganisha bure.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved