logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jada Pinkett kushtaki aliyedai Ex wake Will Smith ni shoga na ana 'uume mdogo kama kidole'

Bilaal anatajwa kuwa msaidizi wa zamani wa Will Smith.

image
na Davis Ojiambo

Burudani17 November 2023 - 09:12

Muhtasari


  • • Alisema, "Wacha niseme hivi, ni ujinga, sawa? Na ni upuuzi. Na huyu ni mtu ambaye alijaribu kutulaghai pesa ambayo haikufanya kazi.."
Will SMith na Jada Pinkette

Jada Pinkett Smith amezungumza kumtetea mume wake Will Smith, akisisitiza kuwa watamshtaki Brother Bilaal, ambaye alitoa tuhuma za kumdhalilisha kingono dhidi yake.

Hivi karibuni mwigizaji huyo alionekana kama mgeni kwenye Klabu ya The Breakfast, ambapo alitangaza maoni yake kuhusu madai ya Bilaal, ambaye alidai kuwa aliwahi kuwafumania Will Smith na rafiki yake Duane Martin wakifanya mapenzi kinyume na maumbile.

Alisema bila shaka watamchukulia hatua za kisheria kwa kauli zake ovu.

Pinkett-Smith pia aliongeza kuwa Bilaal aliwahi kujaribu kuwanyang'anya baadhi ya pesa kwa misingi, hivyo bila shaka wangeshtaki.

Alisema, "Wacha niseme hivi, ni ujinga, sawa? Na ni upuuzi. Na huyu ni mtu ambaye alijaribu kutulaghai pesa ambayo haikufanya kazi. Tutachukua hatua za kisheria kwa sababu ni jambo moja kuwa na maoni yako. kuhusu mtu fulani kuliko kutunga hadithi mbaya tu. Hilo linaweza kutekelezeka, kwa hivyo tutashughulikia hilo."

Muda mfupi baadaye, alifuatwa na paparazi kutoka TMZ ambaye aliuliza maoni yake juu ya madai hayo ni nini, na akasema tena kwamba wangeshtaki.

Haya yanajiri baada ya Bilaal kutoa matamshi yake wakati wa mahojiano na Tasha K mnamo Jumanne, Novemba 14, 2023, akiita kile alichokiona 'mauaji.'

Bilaal anatajwa kuwa msaidizi wa zamani wa Will Smith.

Kwa maneno yake, "Nilifungua mlango wa chumba cha kubadilishia nguo cha Duane, na hapo ndipo ninapomuona Duane akifanya mapenzi na Will. Kulikuwa na kochi, na Will alikuwa ameinama juu ya kochi, na Duane alikuwa amesimama na kumuua, na kumuua. Yalikuwa ni mauaji mle ndani. Ninaweza kukuambia kinachoendelea ndani; kutoka kwa mtu mwingine yeyote,"

Kando na hayo, pia alisema kuwa Smith ana uume mdogo. Kufuatia hayo, mtandao ulienda wazimu kwa madai yake, na kumwita Smith 'shoga.'


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved