logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond Platnumz ahisi kutumiwa uchawi nyumbani kwake popo akining'inia mlangoni

“Jamani, nimefika hapa, nakutana na popo eti, jamani inabidi sasa hiyo video tusitoe kesho,”

image
na Davis Ojiambo

Burudani07 February 2024 - 06:54

Muhtasari


  • • Kwa kawaida, wabongo wanaamini sana katika uwepo wa uchawi na nguvu za kishirikina katika baadhi ya vitu na matukio.
Diamond atumiwa popo

Msanii anayetajwa kama mburudishaji bora kutoka Tanzania, Diamond Platnumz ameonesha kushtushwa kwake baada ya kurudi nyumbani na kumkuta popo kaning’inia katika mlango wa nyumba yake.

Msanii huyo alichapisha video hiyo kwenye insta story yake na kuonesha wasiwasi akisema kwamba pengine ametumiwa mkosi au uchawi katika nyumba yake kwa njia ya popo.

Kwa Maelezo ya Diamond amesema hakuwa popo wa kawaida Ni wakichawi hivyo ametumwa kwasababu Alitangaza kuachia Video ya Nyimbo yake Mpya Leo saa 10:00 am Asubuhi.

“Jamani, nimefika hapa, nakutana na popo eti, jamani inabidi sasa hiyo video tusitoe kesho,” alisikika akisema kwa sauti iliyojaa wasiwasi.

Hapo hapo mmoja wa watu wake alichukua mkwaju mrefu na kujaribu kumuondoa popo yule huku wenzake wakimtahadharisha kuwa makini kwani popo mwenyewe kwa maelezo yao hakuwa popo wa kawaida kabisa.

Kwa kutumia mkongojo ule, jamaa huyo aliweza kufanikisha kumuondoa popo yule kwenye kizingiti cha mlango huku Diamond na wenzake wakichanganyikiwa na nusura kutoroka popo akiwachanganya.

Kwa kawaida, wabongo wanaamini sana katika uwepo wa uchawi na nguvu za kishirikina katika baadhi ya vitu na matukio.

Hii ndio sababu kubwa kwa nini idadi kubwa ya waganga wa jadi bado wamo katika shughuli zao kwa wingi nchini humo, Waswahili hao wakiamini kwamba katika kila jambo baya linalowatokea kuna mkono wa mtu, kwa hiyo suluhu ni kwa mganga wa jadi.

Hata hivyo, taasisi za kisheria na serikali kwa muda mrefu zimekuwa zikisisitiza kwamba suala la uchawi ni la kufikirika tu wala halipo kwani ni vigumu kwa mtu kutoa uthibitisho tosha wa kushawishi mahakama kuhusu uchawi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved