Mfanyabiashara na mtayarishaji maudhui Mkenya Maureen Waititu kwa mara nyingine tena amevutia hisia za mashabiki wake kwa chapisho lake jipya zaidi.
Mnamo Juni 16, mshawishi huyo alishiriki video yake akitabasamu, ikiambatana na maelezo mafupi ambayo yamezua mijadala miongoni mwa wafuasi wake.
Katika chapisho lake, Maureen alielekeza ujumbe kwa wanaume walio na umri wa miaka 40 na zaidi, akiwashauri kufikiria upya uchaguzi wao wa kuchumbiana.
Alipendekeza kuwa badala ya kuwafuata wanawake wenye umri mdogo, watafute wapenzi ambao wamekomaa vya kutosha kutambua masuala makubwa ya kiafya, kama vile dalili za kiharusi.
"Ikiwa una umri wa miaka 40 na kuendelea, ni wakati wako wa kuacha kuwakimbiza wasichana wadogo na kutafuta mwanamke ambaye anaweza kutambua dalili za kiharusi," Maureen aliandika.
Kauli hii ilijulikana sana kwa sababu ilikuja muda mfupi baada ya Maureen kuchagua kutomtambua baby dady wake, Frankie JustGymIt, katika Siku ya Akina Baba. Ujumbe wake ulio wazi ulionekana kuwaonya wanaume wazee kuhusu mambo yanayofaa yanayoletwa na uzee.
Zaidi ya miaka sita imepita tangu Maureen Waititu alipoachana na baby daddy wake, Frankie JustGymIt.