logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wapenzi wa zamani wa Diamond, Hamisa na Wema sasa watoshana kwa idadi ya followers Instagram

Hamisa Mobetto sasa amekuwa wa pili kufikisha idadi hiyo ya wafuasi milioni 11.5.

image
na Davis Ojiambo

Burudani19 June 2024 - 13:53

Muhtasari


  • • Diamond mwanzo alichumbiana na Wema Sepetu kabla ya kuachana na baadae akachumbiana na Hamisa Mobetto.
Wema na Hamisa

Hamisa Mobetto sasa amemfikia mwenzake Wema Sepetu katika idadi ya wafuasi kwenye mtandao wa Instagram.

Kwa muda mrefu, Wema Sepetu  amekuwa mtumizi wa Instagram kutoka nchini Tanzania mwenye wafuasi wengi katika mtandao huo akiwa na wafuasi milioni 11.5.

Hamisa Mobetto sasa amekuwa wa pili kufikisha idadi hiyo ya wafuasi milioni 11.5.

Itakumbukwa kwamba kinachowavutia wengi ni ukweli kwamba wawili hao waliwahi kuwa wapenzi wa msanii mkubwa nchini humo, Diamond Platnumz ambaye pia ndiye mtu wa pekee kutoka Tanzania mwenye wafuasi wengi, Zaidi ya milioni 17.

Diamond mwanzo alichumbiana na Wema Sepetu kabla ya kuachana na baadae akachumbiana na Hamisa Mobetto ambaye walipata mtoto pamoja, mtoto ambaye amekuja kuibuka kuwa wa kuvutia mambo mengi mitandaoni wengi wakihoji uhalali wa Diamond kuwa babake wa kumzaa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved