logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tuko pamoja! Ujumbe wa Eric Omondi kwa waandamanaji wa kupinga mswada wa fedha

Licha ya kukosekana kwenye maandamano dhamira ya Omondi kwa sababu hiyo ingali thabiti.

image

Burudani20 June 2024 - 12:05

Muhtasari


  • Ujumbe wake uliandamana na mahojiano ya awali kwenye runinga ya Citizen ambapo aliionya serikali kwa hisia kali kuhusu madhara iwapo Mswada wa Fedha utapitishwa.
Eric Omondi

Mcheshi maarufu  Eric Omondi ameelezea uungaji mkono wake usioyumba kwa Wakenya wanaopinga Mswada tata wa Fedha wa 2024.

Licha ya kukosekana kwenye maandamano dhamira ya Omondi kwa sababu hiyo ingali thabiti.

Kwa sasa Omondi anajiandaa kumzika mdogo wake, Fred, ambaye alipoteza maisha yake katika ajali ya barabarani.

Omondi, anayejulikana kwa msimamo wake mkali dhidi ya sera za serikali, amekuwa mtu mashuhuri katika maandamano yanayoendelea.

Amekosa maandamano ya hivi majuzi lakini anaendelea kupata uungwaji mkono kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa mengine.

"Tuko Pamoja. go soldiers Wacha nimalize nikam," Omondi alichapisha, akionyesha mshikamano wake na waandamanaji.

Ujumbe wake uliandamana na mahojiano ya awali kwenye runinga ya Citizen ambapo aliionya serikali kwa hisia kali kuhusu madhara iwapo Mswada wa Fedha utapitishwa.

“Nataka niongee na Serikali ya siku na Rais, haitakuwa biashara kama kawaida endapo muswada wa fedha utapita, Serikali haitakuwa na amani, tunaenda mitaani, hawa vijana wapo. atasimama,” alisema Omondi.

Maandamano hayo ambayo awali yalijiri jijini Nairobi, sasa yameenea katika maeneo mbalimbali ya nchi, ikiwemo Mombasa, Eldoret, Kericho, Nakuru, Nyeri na Kakamega miongoni mwa mengine.

Katika mwaka uliopita, Eric Omondi ameibuka kama sauti inayoongoza kukosoa sera za serikali huku pia akishiriki katika juhudi za uhisani.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved