logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dorea Chege aeleza kwa nini anafurahia kuchumbiana na DJ Dibul

Kulingana na mwigizaji huyo, anampenda mpenzi wake, Dj Dibul, na anamuamini kabisa

image
na Davis Ojiambo

Burudani28 June 2024 - 12:45

Muhtasari


  • •Kulingana na mwigizaji huyo, anampenda mpenzi wake, Dj Dibul, na anamuamini kabisa kwa sababu hajawahi kumpa sababu ya kumtilia shaka.
  • •Alikiri kupokea meseji nyingi kutoka kwa wasichana wakijaribu kuchafua jina la mpenzi wake ili waachane, lakini amekuwa akiwafukuza kwa sababu anamwamini mwanaume wake.

Mwigizaji wa Kenya na mshawishi wa chapa Dorea Chege, anayefahamika kwa jina la kisanii ‘Maggie’, amefichua ni kwa nini yuko sawa na kuchumbiana na DJ.

Kulingana na mwigizaji huyo, anampenda mpenzi wake, Dj Dibul, na anamuamini kabisa kwa sababu hajawahi kumpa sababu ya kumtilia shaka.

“Ninamwamini kwa sababu hajawahi kunipa sababu ya kutomwamini, hata siku moja.” Alisema.

Alikiri kupokea meseji nyingi kutoka kwa wasichana wakijaribu kuchafua jina la mpenzi wake ili waachane, lakini amekuwa akiwafukuza kwa sababu anamwamini mwanaume wake.

“Amelelewa vizuri; Huwa napata DM nyingi sana kutoka kwa wasichana wengi, sijui niliona DJ Dibul wapy, kwa hiyo sijali sana kwa sababu ninamwamini.” Dorea Chege alieleza.

Aliendelea kutoa ufahamu juu ya maswala ya uhusiano na kupata mwanaume mwaminifu, akishauri umma kwamba ni kweli unapata kile ulichodhihirisha wakati wote na kwamba binadamu ni zao la kile unachofikiria.

"Kuna wanaume waaminifu. Wako ni mentality yako, ukiendelea kushawishi akili yako kwamba hakuna mtu mwaminifu, hutawahi kumpata,. Itabidi uwe na mafikira tofauti.” Alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved