logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“I’m unbwogable!” Larry Madowo ajibu vitisho kisa kusema hajui wanahabari wenza maandamanoni

“Mimi ni unbwogable,” Madowo alisema katika moja ya chapisho lake Facebook.

image
na Davis Ojiambo

Burudani30 June 2024 - 05:33

Muhtasari


  • • Hata hivyo, Madowo katika machapisho yake ameonesha ujasiri wake akisema kwamba hayuo tayari kumezeshwa woga.

Mwanahabari wa Kenya anayefanya kazi kwenye shirika la habari la kitaifa, CNN Larry Madowo amefichua kwamba baadhi ya watu wameanza kumtishia maisha katika DM zake kwenye mitandao ya kijamii.

Madowo alionyesha baadhi ya jumbe za vitisho kutoka kwa Wakenya ambao walionesha ghadhabu na yeye kutokana na kisa kilichojiri Alhamisi wiki jana wakati wa maandamano jijini Nairobi.

Katika kisa hicho, Madowo alikuwa na makumi ya waandishi wengine wa habari kutoka humu nchini, wengine wakiwa chipukizi ambao walikuwa wanahaha kunasa matukio ya maandamano.

Lakini haikuwa rahisi kwa sababu polisi walikuwa wanazuia baadhi ya matukio kunaswa na watu wasiojulikana kama ni wanahabari.

Katika zogo hilo, polisi walimkabili Madowo na kumtaka kueleza hao aliokuwa nao na Madowo alijibu polisi kwamba hakuwa anawajua bali kila mtu alikuwa akifanya kazi yake kivyake, wala si washirika wake wala wa CNN.

Hili lilipelekea polisi kuwafukuza waandishi hao chipukizi kwa kutojitambua vilivyo.

Tukio hilo lilivutia maoni kinzani katika mitandao ya kijamii, baadhi wakimtuhumu Madowo kwa kushindwa kuwatetea wanahabari wenza huku wengine wakisimama upande wake na kusema kila mmoja alikwenda kunasa matukio ya maandamano kivyake hivyo haikuwa lazima Madowo kuwatetea kwa polisi.

Siku mbili baadae, Madowo ameonyesha watu kufurika katika DM zake na kumtumia jumbe za matusi na za kumtishia kwa kuwaacha wanahabari chipukizi wa Kenya kudhalilishwa na polisi wakati wa maandamano badala ya kuwatetea.

Hata hivyo, Madowo katika machapisho yake ameonesha ujasiri wake akisema kwamba hayuo tayari kumezeshwa woga.

“Mimi ni unbwogable,” Madowo alisema katika moja ya chapisho lake Facebook.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved