logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ng’ang’a amsuta Mbunge Mohamed Ali kuhusu mswada tata wa Fedha

Mchungaji alikumbuka maisha ya zamani ya Mohamed Ali kama mwandishi wa habari.

image
na Davis Ojiambo

Burudani01 July 2024 - 09:39

Muhtasari


  • •Mchungaji alikumbuka maisha ya zamani ya Mohamed Ali kama mwandishi wa habari, ambapo alijulikana kwa uchunguzi na msimamo mkali juu ya haki za binadamu na utawala bora.
  • •Matamshi yake yanakuja huku kukiwa na hasira ya umma dhidi ya wabunge waliounga mkono Mswada tata wa Fedha wa 2024.

Mhubiri James Maina Ng’ang’a wa Neno Evangelism Centre amemsuta mbunge wa Nyali Mohamed Ali, almaarufu Jicho Pevu.

Mhubiri huyo mwenye utata alimtaka ajieleze kwa kuunga mkono Mswada wa Fedha wa 2024, ambao Wakenya wengi wameupinga.

Katika video moja kwenye mahubiri yake, Mchungaji Ng’ang’a alimkosoa vikali mbunge huyo, akimlaumu vikali kwa kubadilisha mienendo yake baada ya kuingia kwa siasa.

Mchungaji alikumbuka maisha ya zamani ya Mohamed Ali kama mwandishi wa habari, ambapo alijulikana kwa vipande vyake vya uchunguzi na msimamo mkali juu ya haki za binadamu na utawala bora.

Wakati wa taaluma yake ya uandishi wa habari, Ali alipata jina Jicho Pevu kutoka sehemu yake ya ripoti za uchunguzi na Kuwa mtu anayependwa sana na Wakenya.

“Jicho Pevu sasa jiangalie mwenyewe Ile jicho pevu ulikuwa nayo ilienda wapi sasa. Mbona huwezi kueleza hii kiinaendelea.

Wewe Jicho Pevu ona jicho pevu hii utuelezae nyinyi mmenunuliwa mmepewa pesa ngapi.”

“Hata nimeona watu wako wanasema ulivote yes na wewe ni jich pevu.

Jicho pevu sasa jiangalie mwenyewe tumbo lako. Waongo hao!” Mchungaji Ng’ang’a alifoka.

Kasisi Ng’ang’a aliwaambia watu wajaribu kumkabili, akidai kwamba walinzi wao wangewageuka.

“Ukinijaribu, utajiua. Mlinzi wako atakupiga risasi,” Ng’ang’a aliongeza.

Matamshi yake yanakuja huku kukiwa na hasira ya umma dhidi ya wabunge waliounga mkono Mswada tata wa Fedha wa 2024, ambao wengi wanaona kuwa haujali masaibu ya Wakenya.

Licha ya maandamano makubwa, wabunge wengi walipitisha mswada huo katika hatua zote.

Ni baada tu ya Wakenya kadhaa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa ndipo Rais, ambaye hapo awali aliunga mkono mswada huo, aliamua kuukataa kuutia saini.

Zaidi ya hayo, Rais alisema kuwa uamuzi wake ulitokana na upinzani mkali kutoka kwa Wakenya dhidi ya mapendekezo ya kodi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved